• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yapokea Bilioni 24 kwa ajili ya Utekelezaji Mirada ya TASAF

Posted on: October 27th, 2021

Serikali ya Awamu ya Sita imedhamiria kuinua kaya zenye changamoto ya umasikini kwa kuzijengea uwezo,uelewa na kuziwezesha kukuza uchumi na kuboresha vipato ambapo imetenga sh. bilioni 24.595 za kutekeleza mradi wa kupunguza umasikini mkoani Mwanza.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.Mhandisi Robert Gabriel, wakati akizindua awamu ya nne ya mradi huo miaka mitano wa kupunguza umasikini mkoani humu.

Alisema adhima na dhamira ya serikali ya awamu ya sita ni kuinua kaya zenye changamoto ya uchumi na kuziwezesha kutumia fursa za kuongeza kipato,kukuza uchumi wa kaya,kuboresha huduma za jamii na kuwekeza kwenye maendeleo ya watoto.

Mhe.Mhandisi Gabriel alisema mpango huo wa miaka mitano, kitaifa ulizinduliwa mkoani Arusha, Oktoba 10, mwaka huu, na Waziri wa Utumishi na Utawala Bora, Mohamed Mchengerewa, utatoa ajira za muda kwa kaya za walengwa,itaibuliwa miradi ya miundombinu ya jamii ya kutolea huduma za afya,elimu,barabara,maji safi na salama pamoja na utunzaji wa mazingira.

“Miradi hiyo itatoa ajira za muda kwa jamii na kupata fedha za kuboresha maisha,kuongeza kipato na kuendeleza miundombinu ya afya,elimu na maji,kupata ujuzi na stadi za maisha kwa walengwa,”alisema.

Mhe. Gabriel alisema kuwa wasimamizi wakuu wa miradi hiyo kutoka mkoani waisimamie kwa kufuata miongozo yote ili kuendana na fedha zilizotolewa ambazo kitakuwa kipimo cha uadilifu na uwajibikaji.

 “Tumepewa zaidi ya sh. bilioni 24 kutekeleza miradi ya kupunguza umasikini,naomba tuipongeze serikali na juzi tu Mwanza tumepokea bilioni 22 za kujenga madarasa, hurum ya mama n serikali yake anastahili pongezi nyingi sana maana tumeletwa mzigo wa kutosha hatujawahi kuupata hadi usingizi unakataa,”alisema Mhandisi Gabriel.

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Ladslaus Mwamanga,alisema Mradi huo wa Kupunguza Umasikini Tanzania (TPRPIV) ni dirisha la kuongeza fedha kwenye mapungufu ya miradi ya miundombinu ya afya,elimu,maji na barabara zitakazotumiwa na jamii, ambayo itatekelezwa kwenye mikoa mitano ya Njombe,Arusha,Geita,Mwanza na Simiyu.

Alisema madhumuni makubwa ya kutekeleza mpango huo wa awamu ya 4 ni kupunguza umasikini wa wananchi ili watu waende kwenye vituo afya kujiimarisha kiafya na awamu ya pili itahusisha ujenzi wa madarasa na nyumba za watumishi ili kuziba mapengo katika maeneo mengine ya mradi.

“Kutakuwa na miradi ya ajira,vitaanzishwa vikundi vya watu 15 na kupewa sh. milioni 15 za kuanzisha miradi ya kujiongezea kipato, na hiyo ndiyo mikakati ya TASAF na ndio maana ya kujenga uelewa wa pamoja kati ya viongozi wa serikali,wanasiasa na watalaamu ili wafikishe ujumbe sahihi kwa wananchi waje na vipaumbele vyao,”alieleza Mwamanga.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.