• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yaweka mikakati ya Ufaulu mitihani darasa la saba

Posted on: August 13th, 2019


Serikali mkoani Mwanza  imewakutanisha maofisa elimu wilaya, kata na wakuu wa shule kwa ajili ya kufanya tathimini mitihani ya darasa ya saba  na kubaini baadhi ya changamoto zinazoikabili elimu Mkoani hapo.

Kikao hicho kimekusudia kupata majibu kutoka kwa maofisa hao kueleza sababu ya baadhi ya halmashauri kutofikia asilimia 90 ya ufaulu ambao ni lengo la mkoa huo.


Kwa mujibu wa takwimu za mkoa  huo zinaonyesha  halmashauri ya Ilemela ilifikia asilimia 98.3,  Sengerema 97.1,  Misungwi 96.6, Jiji la Mwanza 95.2, Magu 92, Ukerewe 85.4, Kwimba 84.6 na Buchosa 80.5.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungua kikao na maofisa hao, Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Michael Ligola alisema lengo ni kuweka mikakati na kutatua changamoto  zilizopo ili kila halmashauri iweze kufikia  asilimia 90 ya ufaulu katika mitihani ya kitaifa.


Ligola alisema katika mitihani  ya majaribio iliyofanyika ngazi ya mkoa, baadhi ya halmashauri   ziliweza kufikia asilimia 90 lakini nyingine  zilifikia asilimia 80, hivyo kitendo cha kuwakutanisha maofisa elimu wilaya, kata na wakuu wa shule   ni kutaka kuwa katika mstari unaofanana.


Ligola alisema Julai 17-18 mwaka huu kulifanyika mtihani wa mjaribio mkoa ambapo wanafunzi 68,356 kutoka shule za msingi 944  walitarajiwa kufanya  lakini  waliofanya mitihani  hiyo ni  67,322 kati ya hao wavulana  31,789 mna wasichana 35,533 na asilimia 98.3.


Alisema wanafunzi ambao hawakufanya mtihani huo  1,034 kati ya hao wavulana ni 347 na wasichana 687 sawa na silimia 1.5, hivyo alisema kiwango hicho cha wanafunzi wasiofanya mtihani ni kikubwa na kinapaswa kutafutiwa suluhisho.


“Lengo la Serikali ni ufaulu uwe asilimia 100 kitaifa lakini hapa Mkoa wa Mwanza tulijiwekea malengo yetu yawe asilimia 90 au zaidi,sasa katika  mitihani ya majaribio tuliyofanya ngazi ya mkoa baadhi ya halmashauri zimeonekana kutofikia lengo letu, sasa nimelazimika kuwakutanisha ili kila mmoja aseme kilichomkwamisha hali hiyo kujitokeza.


“Bila shaka kila mmoja atasema na baadaye tutajadiliana kuona wapi panatakiwa kurekebishwa ili mtihani ujao tuweze kufanya vizuri, kwa habati nzuri Mkoa wa Mwanza hali ya taaluma siyo mbaya hivyo matarajio yetu  shule zilizofaya vibaya tutasikia sababu zao ni zipi na tutaelezwa wale waliofanya vizuri wao walifanya nini,”alisema.


Kwa upande wa Afisa Elimu Kata ya Nyamanoro Wilaya ya Ilemela, Iloze Ngereza alisema licha ya eneo lake kufanya vizuri katika mitihani ya majaribio lakini changamoto kubwa iliyopo ni utoro wa wanafunzi.


“Unajua walimu wanaweza kuwa wanafundisha vizuri sana  lakini changamoto inakuja ya utoro wa wanafunzi, hawa watoro ambao hawahudhulii masomo kila siku wanajitokeza siku ya mitihani na ndiyo wanaofanya vibaya na kusababisha  kushusha ufaulu.


“Ukichumnguza wale wanaokuwa wanahudhuhulia kila siku wanafanya vizuri lakini wanaangushwa na wale watoro, mfano katika kata yangu ukifuatilia watoro katika shule zote unakuta wanafikia kati ya 300 hadi 400,  ndiyo maana tunafikia hatua tunawafuatilia sambamba na wazazi wao,”alisema.


Naye Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Bujingwa iliyopo Wilaya ya Kwimba, Mathias Tito amesema shule yake ni miongoni kwa shule zilizofanya vibaya hivyo kikao hicho kitasaidia kubadilishana mbinu zitakazofanya halmashauri zote kuwa katika mstari mmoja wa ufaulu wa asilimia 90 kama malengo ya mkoa yalivyoainishwa.


“Unajua shule yangu ipo katika mazingira mabaya, ipo mbali ambapo walimu wanasafiri muda mrefu lakini kama kungekuwa na nyumba za kutosha   zingesaidia kuishi pale pale, hata hivyo wanapokuwa shuleni pale wanashinda njaa hii ni changamoto sana,’”alisema.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.