• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWENGE WA UHURU WAWASILI MWANZA, RC MTANDA AUPOKEA

Posted on: October 6th, 2024

MWENGE WA UHURU WAWASILI MWANZA, RC MTANDA AUPOKEA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo  06 Oktoba 06, 2024 ameupokea Mwenge wa Uhuru ukitokea Mkoani Geita tayari kwa kutembelea, kukagua, kuweka mawe ya msingi na kuzindua miradi 58 ya maendeleo yenye thamani ya zaidi ya Bilioni 98.

Akizungumza kwenye mapokezi hayo yaliyofanyika kwenye kijiji cha Nyamadoke Halmashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema Mhe. Mtanda amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika wilaya 7 na Halmashauri 8 katika umbali wa zaidi ya kilometa 649.

Ameongeza kuwa Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani Mwanza utaifikia miradi lukuki yenye viwango katika sekta za maji, elimu, afya, kilimo na miundombinu kwani Mkoa huo unaochangia pato la taifa kwa asilimia 7.2 una uchumi imara na kwamba wakimbiza mwenge wataishi kwa amani kwani kuna utulivu.

Akizungumzia masuala ya lishe, Mhe. Mtanda amesema Mkoa huo umeendelea kuimarisha kwenye eneo hilo kwa kutekeleza afua mbalimbali kama kutoa elimu na kuimarisha lishe bora kwa chakula cha watoto shuleni na imesaidia kupunguza ukondefu kutoka asilimia 3 mwaka 2017 hadi asilimia 1 mwaka huu.

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava amesema ubora wa miradi utaonekana kwenye thamani ya fedha zilizotumika na huo utakua ndio msingi wa ukaguzi na kwamba taarifa sahihi za miradi zitachagiza ushindi kwenye ukaguzi.

Wakati huo huo Mhe. Mtanda amemkabidhi Mwenge wa Uhuru Mhe. Seni Ngaga Mkuu wa Wilaya ya Sengerema kwa ajili ya kukimbiza mwenge wa uhuru kwenye halmashauri ya Buchosa leo Oktoba 06 2024.

Kauli mbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka huu ni "Tunza mazingira, "Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Ujenzi wa Taifa Endelevu".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.