• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI WA VIZIMBA NYAMAGANA

Posted on: October 9th, 2024

MWENGE WA UHURU WAZINDUA MRADI WA UFUGAJI SAMAKI WA VIZIMBA NYAMAGANA


Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Eliakim Mnzava amezindua mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba wa kikundi cha Vijana kinachojulikana kama Vijana Agro wenye thamani ya Tshs. Milioni 206 hadi kuanza uzalishaji.

Akizungumza na wananchi mara baada ya ukaguzi kwenye eneo la mradi huo uliopo katika mtaa wa Kisoko, kata ya Luchelele wilaya ya Nyamagana leo  Oktoba 09, 2024 Mnzava ameipongeza Halmashauri ya Jiji hilo kwa kuwakopesha vijana hao 7 kiasi cha tshs. milioni 150 hali iliyowafanya wapate na kupelekea kutengeneza miundombinu.

Aidha, amewataka vijana hao kuweka nidhamu kwenye utekelezaji wa mradi huo ili waendelee kuzalisha na kuuza samaki ambao soko lake ni kubwa sana kwa sasa na akawataka kuhakikisha wanafanya marejesho ya mkopo huo illi vijana na makundi mengine waweze kupata mkopo pia.

Akitoa taarifa ya mradi huo Mwenyekiti wa kikundi ndugu Christopher Gugu amesema mkopo huo pamoja na mtaji wao wa milioni 56 walizokua nazo hapo awali zimewasaidia kutengeneza vizimba 3 vikubwa, ununuzi wa boti na injini yake, mitumbwi 2, mashine 2 HP 15, tani 21.8 za chakula cha samaki, vifaranga pamoja na ujenzi wa stoo ya kuhifadhia chakula cha samaki.

Aidha, ametaja manufaa waliyoyapata kutokana na mradi huo kama kuongeza mapato ya kikundi kwani uvunaji wa awamu mbili na umewapatia milioni 86.4 na kuwafanya waanze kurejesha mkopo huo pamoja na kuongeza boti kutoka 3 hadi 6 na kwamba wameajiri vijana 6 nje ya vijana 7 waanzilishi.

Mwenge wa Uhuru Wilayani Nyamagana umetembelea mradi wa maji safi Butimba wenye thamani ya bilioni 71.9 unaotekelezwa na programu ya maji na Usafi wa mazingira ambapo baada ya ukaguzi kiongozi wa mbio hizo ameipongeza Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa mazingira (MWAUWASA) kwa kuongeza upatikanaji wa huduma hiyo kwa jamii.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.