• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Prof Mkenda ahitimisha ziara ya kikazi kanda ya ziwa, aridhishwa na utekelezaji wa miradi

Posted on: July 6th, 2023



Prof Mkenda ahitimisha ziara ya kikazi kanda ya ziwa, aridhishwa na utekelezaji wa miradi*


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolph Mkenda ameendelea na ziara ya siku tatu katika Mikoa ya kanda ya ziwa iliyojikita katika ukaguzi wa Miradi iliyo chini ya Wizara hiyo ambapo leo Julai 06, 2023 amefika Mkoani Mara akitokea Mkoani Mwanza.

Akizungumza na Uongozi na watumishi wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere cha Kilimo na Teknolojia kwenye Kampasi ya Oswald Mang'ombe, Prof Mkenda amesema amefurahishwa na Ukarabati wa Miundombinu ya chuo hicho ambao umeonesha nia ya dhati ya kutaka kudahili wanafunzi mwanzo wa muhula wa mwaka 2023/24.

"Tumezunguka kote, tumekagua na kwakweli tumeridhika na nina imani kwamba tukienda hivi basi tutakua tayari kupokea wanafunzi kwa ajili ya masomo ndani ya mwaka huu wa masomo na niwape tu taarifa kuwa tayari wajumbe wa baraza la Chuo wameshapatikana ambapo Mhe. Mizengo Pinda Waziri Mkuu Mstaafu ndiye Mkuu wa chuo hiki." amesema Prof Mkenda.

Amesema Serikali imeamua kutenga zaidi ya Bilioni 2.6 kwa ajili ya ukarabati huo ili kuinua Sekta ya Kilimo nchini na kwamba chuo hicho kitaleta alama isiyofutika kwenye mageuzi ya Kilimo na Teknolojia nchini na ametumia wasaa huo kutoa rai kwa Uongozi kuanza kwa vitivo vinavyobuniwa vizuri ili kutoa umahiri uliokusudiwa kwa vijana.

Akitoa salamu za Mkoa wa Mara, Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Said Mtanda ameihakikishia Wizara ya elimu ushirikiano ili kuhakikisha kinakarabatiwa na kuwa chuo cha mfano nchini ikiwa ni katika kuenzi pia tunu ya asili ya Baba wa Taifa Hayati Mzee Nyerere na kwamba kitakapokamilika kitachochea ubunifu, umahiri katika sekta ya kilimo na hata Utalii katika ukanda huo.

Mhe. Jumanne Sagini, Naibu Waziri wa Mambo ya ndani ya nchi ametumia wasaa huo kuishukuru wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa kuwaletea Butiama Miradi mbalimbali kwenye wilaya hiyo na ametoa rai kwa Uongozi wa Chuo hicho kuhakikisha Ukarabati unaanza mara moja na kukarabati chuo kwa ubunifu.

"Katika zoezi la Ukarabati Mhe. Waziri tumezishirikisha taasisi za wenzetu kama vile VETA, TBA, Bonde la Ziwa Victoria, Halmashauri ya wilaya ya Butiama na Ruwasa ambao wametuhakikishia kuwa tutapata maji ya kutosha kuhudumia chuo hiki." Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Lesakit Mellau


Naye, Prof. Msafiri Jackson ambaye ni Kaimu Mkuu wa Chuo Utawala, fedha na Mipango amebainisha kuwa Mradi wa Ujenzi wa Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Mwalimu Nyerere Kampasi ya Butiama utasaidia kuimarisha mafunzo ya kujifunzia na Ufundi Stadi.


Katika wakati mwingine Prof. Mkenda amefika  kwenye kijiji cha Rwamkoma na kukagua eneo Maalum ambalo itajengwa miundombinu ya Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Mwalimu Nyerere tawi la Butiama ambapo zaidi ya Bilioni 44.5 zitatumika chini ya Mradi wa Higher Education Econ. Trans (HEET) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.