• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

Posted on: September 27th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema amefurahishwa na programu ya Wanawake na Samia inayolenga kutoa ujuzi na uwezo wa kusimamia fani mbalimbali yenye lengo la kukuza uchumi na kipato kwa Wanawake na Wasichana.

Mkuu wa Mkoa amesema programu hiyo ni muhimu na kisha kutoa wito kwa watoto wa kike kuchangamkia fursa hiyo ili wanufaike na sio kuishia kutazama tu, amesema kwa sasa kila kijana ana vyeti vya taaluma lakini ni wachache walioajiriwa na serikali hivyo kundi kubwa ambalo halijaajiriwa Serikali inalinasaidia kupata taaluma ya ujuzi ili waweze kujiajiri na kuajiriwa.

Mkuu wa Mkoa amebainisha hayo leo Jumamosi tarehe 27, Septemba 2025 wakati akizindua Programu ya Mafunzo ya Wanawake na Samia katika Mkoa wa Mwanza iliyofanyika katika Viwanja vya michezo VETA Mkoa wa Mwanza.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa amesema anatamani kuona kunakuwepo na majukwaa ya Wahitimu kutoka Vyuo mbalimbali ili wasikilizwe na kisha kupewa elimu ya fani tofauti tofauti kwa kuwa serikali ina mikopo na mitaji hivyo wanaweza kupewa elimu ya kujiunga na vikundi ili waweze kunufaika na kuanza kuingiza kipato.

“Na hapa lazima tubadili fikra zetu, ukiwa unakaa unasema huwezi kufanya jambo hili kwa kuwa jambo hili sio nililolisomwa inakua ni kupoteza muda”. Mhe. Mtanda.

“Hapa Mwanza kuna vitu vingi na hata vijana wanaweza kujiunga na kuunda vikundi wakawa na wazo lao hata la kufanya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba wakati wanasuburi ajira ambazo ziko kwenye fikra zao lakini waanze kujikwamua na kuchangia pato la Taifa.” Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Akisoma taarifa ya Programu hiyo, Mkuu wa Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Mwanza Bw. Thomas Kasele amesema Programu ya Wanawake na Samia ni programu inayodhaminiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo lengo lake ni kuwawezesha wanawake kupata uwezo na ujuzi wa kujiajiri na kuajiriwa ili waweze kujikwamua na umaskini.

“Mkoa wa Mwanza jumla ya Wanawake 2500 wamedahiriwa katika fani mbalimbali ambapo kwa VETA Mwanza ni wanawake 2200, VETA Kwimba 18 na Ukerewe 83”. Amebainisha Bw. Kasele.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • WANANCHI WAASWA KUBADILI MTINDO WA MAISHA ILI KULINDA AFYA YA MOYO

    September 29, 2025
  • PROGRAMU YA WANAWAKE NA SAMIA SI YA KUBEZWA NI FURSA YA KUKUA KIUCHUMI - RC MTANDA

    September 27, 2025
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI KUTOKA WIZARA YA MADINI

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.