Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Rais Magufuli kutua Mwanza kutatua changamoto za ALAT

Posted on: July 19th, 2019


Mhe.Rais Dkt.John  Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi   katika mkutano mkuu wa 35 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini (ALAT) utafaokafanyika  jijini Mwanza kwa siku tatu huku kilio kikubwa kwa halmashauri ni kunyang’anywa vyanzo vya mapato na posho za madiwani.

Akizungumza na waandishi wa habari , Mwenyekiti wa ALAT Taifa, Gulamhafeez Mukadam alisema mkutano huo unatarajiwa hudhuriwa na wajumbe na viongozi waalikwa zaidi ya 700  ambapo mada na changamoto mbalimbali zinazozikabili halmashauri zote nchini zitawasilishwa na kujadiliwa kwa kina na kutoa mapendekezo kwa Serikali Kuu.

Mukadam alisema mkutano huo ambao wajumbe wake ni wakurugenzi wote nchini, mbunge mmoja kwa kila mkoa, madiwani na viongozi wengine waalikwa, utatoa fursa kwao kuileza Serikali  hali halisi ya namna halmashauri zinavyofanya kazi katika mazingira magumu.

Pia alisema watatumia nafasi hiyo kuwasilisha kilio chao cha muda mrefu juu ya maslahi ya madiwani pamoja na viongozi wa Serikali za mtaa wakiwamo wenyeviti na wajumbe wao ambao wanafanya shughuli nzito ya kuwahudumia wananchi lakini mwisho wa siku wanaachwa patupu.

Mukadam alisema hivi sasa halmashauri nyingi zimeyumba kutokana na kukosa vyanzo vipya vya mapato lakini aliishukuru Serikali kuu kwa kutoa pesa kwa baadhi ya halmashauri pale inapojitokeza kuwapo na uhitaji wa lazima kama ujenzi wa zahanati.

“Kumbukeni ALAT ni umoja wa halmashauri ya miji na majiji Tanzania sasa tunapokuja kukutana hivi ni jambo kubwa sana ndio maana tumemwalika Mhe. Rais Magufuli ili tumwambie halisi halisi ilivyo huku chini, tutamweleza juu ya mabaya na mazuri yaliyopo ikiwa lengo ni kusukuma maendeleo ya halmashauri zetu.

“Madiwani tunayo madai mengi sana yakiwamo kupandishwa kwa posho zetu na hiki ni kilio cha muda mrefu sana, pia hivi sasa halmashauri zimenyang’anywa vyanzo vyake na zinafanya kazi katika mazingira magumu, ingawa lengo la serikali ni zuri kwamba fedha zote zikusanywe pamoja na zitakuwa zikirejeshwa kwetu.

“Utakumbuka posho za madiwani zinalipwa kutokana na fedha za ndani, sasa kama vyanzo vya mapato ndiyo hivyo tumenyang’anywa sasa inakuwa vigumu madiwani kupata stahiki zao kwa wakati, naweza kusema pendekezo letu ni kutaka mzigo huu ubebwe na serikali kuu, maana huku halmashauri zipo taabani.

Hata hivyo aliziomba halmashauri ambazo hazijawasilisha michango yao ziweze kufanya hivyo ingawa wanatambua kwamba  mifumo ya pesa imefungwa.Aliongeza kuwa  mkutano huo utaleta fursa kwa Mkoa wa Mwanza na kuwataka wafanyabishara kuchangamkia mwanya huo waweze kufaidika.

Alisema mpaka sasa wameanza kuwapokea viongozi mbalimbali wa Serikali na huku akiwataka wajumbe wa ALAT kujisajili katika ofisi za Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kupatiwa vifaa ili kuondoa usumbufu siku ya mkutano.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.