• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Rais Samia atoa msaada wa chakula kwa vituo vya watoto waishio mazingira magumu Mwanza

Posted on: January 9th, 2024

Rais Samia atoa msaada wa chakula kwa vituo vya watoto waishio mazingira magumu Mwanza


Leo Januari 9, 2024 Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa msaada wa chakula kwa vituo viwili vya watoto waishio katika mazingira magumu na hatarishi Mkoani Mwanza katika wilaya za Nyamagana na Ilemela ikiwa ni zawadi za Sikukuu za Krismasi na na Mwaka Mpya.

Akikakabidhi zawadi hizo kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Daniel Machunda kwenye vituo vya Console kilichopo wilayani Nyamagana na Fonalisco kilichopo Ilemela kwa kila kituo ni mchele kilo 100,maharage kilo 100,mafuta lita 20,mbuzi 1,nyanya tenga 1,juice katoni 3 pamoja na biskuti maboksi 3 vyenye thamani ya Shs 1,700,000

Akizungumza na viongozi wa vituo hivyo pamoja na watoto hao Machunda amesema msaada huo wa Rais ni ishara ya kuendelea kuwakumbusha Serikali inawajali, inawathamini na kuwapenda hivyo wasijione wanyonge au kutengwa na jamii badala yake wadumu katika tabia njema na kuzingatia masomo ili waje kutimiza ndoto zao za kuwa viongozi au wafanyakazi bora wa Taifa hili siku za usoni.

"Nipo hapa mbele yenu kuja kuwaletea salamu za Rais wetu ninazo wasilisha mbele yenu kwa niaba ya mkuu wetu wa Mkoa Mhe.CPA.Amos Makalla amewasihi sana muishi kwa upendo huku mkiwa na imani Serikali ipo nyuma yenu kwa shida na raha hivyo ni wajibu wenu muendelee kujibidiisha katika masomo yenu kama anavyosisitiza Rais wetu kila mmoja asome bila kikwazo chochote,"amesisitiza Machunda wakati akizungumza na watoto hao kwenye kituo cha Fonalisco.

Amebainisha Ofisi ya mkuu wa Mkoa kupitia Idara zake husika itaendelea kuwa bega kwa bega na vituo hivyo kuhakikisha zinatimiza ipasavyo malengo yao ya kuwalea watoto hao kwa kuzingatia mila na desturi zetu ikitambuliwa hao ni hazina ya Taifa.

Kituo cha Console kilichopo wilayani Nyamagana kina  jumla ya watoto 17 na Fonalisco cha Ilemela kina watoto 101 huku baadhi yao wakiwa masomo ya elimu ya juu.

Rais Samia amekuwa na utaratibu wa kutoa zawadi  kwa watoto wote waishio katika mazingira magumu wakati wa sikukuu zote kubwa hapa nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.