• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

Posted on: June 17th, 2025

RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana ameitaka Menejimenti ya halmashauri ya Magu kuja na mpango wa kufuta ufaulu wa daraja la nne na sifuri kwa wanafunzi ili kuhakikisha dhamira ya serikali ya kuboresha elimu inafikiwa kwa wanafunzi kupata daraja la kwanza.

Ndugu Balandya ametoa maagizo hayo leo tarehe 17 juni, 2025 wakati akiongoza baraza maalum la hoja za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa halmashauri hiyo kuishia juni 30, 2024 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa na kubaini ufanisi usioridhisha kwa shule za sekondari na msingi kwa kipindi cha 2021-2023.

"Elimu ndio msingi wa mbeleni, menejimenti ya Magu tafadhali sana daraja sifuri halikubaliki kwa watoto wetu naomba tukajifunze kwenye halmashauri zingine wanafanyaje kuinua ufaulu mathalani Kwimba twendeni tuone wao wamewezaje kwani mazingira yetu hayatofautiani." Amesema Balandya.

Ameongeza kuwa wazazi na walezi wana wajibu wa kuwafundisha stadi za maisha watoto wao kama kufanya usafi wa mazingira na miili yao ili kuwafanya wawe na utayari wa kujibidiisha na kujenga tabia ya kujitegemea kwani tabia bwete husababisha hata kufeli kwenye masomo.

Aidha, amewaagiza Halmashauri ya wilaya ya Magu kuzingatia mahitaji wakati wa uagizaji wa dawa za binadamu kwa ajili ya kusambaza kwenye vituo vya kutolea huduma ili kuepusha kuisha kwa muda wa matumizi na kulazimika kuteketeza.

Amesema ni hasara kuwa na madawa ya zaidi ya milioni tano yaliyoisha muda wake na kulazimika kuteketeza kwani ni uharibifu wa rasilimali fedha na akaliagiza baraza hilo kufuatilia vibali vya kuteketeza dawa hizo ili zisilete madhara kwa watumiaji.


"Hoja zote ambazo hazijatekelezwa ziwekewe mkakati wa utekelezaji wake ili ziweze kufungwa hivyo naagiza muweke vielelezo na viambatanisho vyote ndani ya muda ili kuifanya halmashauri ibaki salama." Amesisitiza Katibu Tawala.


Naye, Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Nje Mkoa wa Mwanza ndugu Henry Chausa amebainisha kuwa 2023/24 halmashauri hiyo ilikaguliwa na kupata hati inayoridhisha na kwamba kuna hoja 46 ambazo zinafanyiwa kazi na kufungwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.