• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA ATOA WITO KWA JESHI LA POLISI KULINDA AMANI KATIKA UCHAGUZI MKUU

Posted on: September 22nd, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana ametoa rai kwa jeshi la polisi na waandishi wa habari kuzingatia maadili, miiko, sheria na taratibu kusimamia uchaguzi Mkuu wa 2025 uwe wa amani.

Ametoa wito huo wakati akifungua mafunzo kwa jeshi la polisi na waandishi wa habari kuhusu haki za binadamu na wajibu waakati wa uchaguzi mkuu 2025 yanayofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Balandya amesema kwa pamoja jeshi hilo na wanahabari wanalazimika kutimiza wajibu wao wa kulinda amani na kuhabarisha umma juu ya mwenendo wa uchaguzi kabla, wakati na baada ya uchaguzi katika kuelekea kuwapata viongozi.

Aidha, ametoa rai kwa makundi hayo kusimamia kampeni za wagombea nafasi mbalimbali zinazoendelea vizuri ili kuhakikisha wananchi wanasikiliza sera kwa utulivu na kujiandaa kwa uchaguzi mkuu ifikapo Oktoba 29, 2025.

Akitoa salamu kwa niaba ya Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Jaji Msataafu Mathew P. Mwaimu Bi. Saumu Mgeni ambaye ni Afisa Uchunguzi -Sheria amesema lengo la mafunzo hayo ni kuongeza uelewa kwa jeshi la polisi na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa kuzingatia sheria wakati wa uchaguzi.

Amesema jeshi hilo lina wajibu wa kusaidia kuzingatia haki na misingi hiyo wakati wote kwa kujiepusha na migogoro isiyo ya lazima na kuhakikisha wanalinda uhuru wa haki na amani kwa kulinda mali za wananchi.

Mafunzo hayo yanatolewa katika Mikoa 14 ya Tanzania Bara na mikoa mitano kwa upande wa Visiwani ambapo kwa upande wa mkoa wa Mwanza mafunzo yanawakutanisha washiriki 60 (Jeshi la Polisi 40 na Waandishi wa Habari 20).

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA ATOA UFAFANUZI JUU YA CHANGAMOTO YA MAJI

    September 23, 2025
  • HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA KUTOLEWA KWENYE MAGEREZA MWANZA

    September 22, 2025
  • RAS BALANDYA ATOA WITO KWA JESHI LA POLISI KULINDA AMANI KATIKA UCHAGUZI MKUU

    September 22, 2025
  • RC MTANDA ASHUHUDIA SAFARI YA KWANZA YA MV NEW MWANZA KWENDA BUKOBA

    September 21, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.