• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Mwanza aagiza huduma ya hewa ya Oxygen kwa Watoto itolewe Vituo vyote vya Afya Mkoani Mwanza

Posted on: May 28th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Ngusa Samike amefanya ziara ya ukaguzi wa Dawa na Vifaa Tiba Vituo vya Afya Wilayani Sengerema na kuagiza Vituo vyote vya Afya viwe na huduma ya watoto chini ya miaka 5 wenye upungufu wa hewa ya Oxygen mwilini.


Katibu Tawala Ngusa akiwa katika Kituo cha Afya Kamanga Wilayani Sengerema amepata taarifa ya huduma hiyo ijulikanayo kitaalam kama TIMCI ambayo ipo kwenye Utafiti hadi mwaka 2024 inatolewa kwenye Vituo 23 Wilayani humo.


"Hii ni huduma muhimu sana watoto wengi wanapozaliwa wanapitia katika changamoto mbalimbali ambazo bila uangalizi wa kitaalam wanapoteza maisha,tufanye jitihada za haraka isambae Wilaya zote za Mkoa wa Mwanza"


Mratibu wa Huduma hiyo inayotibu changamoto zote za upumuaji kwa mtoto Dktr Mujungu Deusdedit amesema mara baada ya Utafiti huo kumalizika watalifanyia kazi agizo la Katibu Tawala kutokana na umuhimu wa Huduma hiyo kutolewa sehemu zote.


Kwa mujibu wa Takwimu hadi mwezi huu jumla ya watoto 6224 wamepimwa wingi wa Oxygen mwilini na 80 wamekutwa na upungufu  huo na kupatiwa matibabu na kunusuru maisha yao.



Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dktr Thomas Rutachunzibwa amesema wanaendelea kuboresha huduma za afya kwenye Vituo na sasa mkazo wameweka upande wa vifaa vya upasuaji.


Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Dktr Saumu Kumbisaga amebainisha Hospitali ya Wilaya ipo katika hatua za mwisho kuanza kutoa huduma kwa Wananchi.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike ametoa agizo Wilayani Sengerema Miradi yote ikamilike kwa wakati, kuwepo na utaratibu sahihi wa matumizi ya dawa na Vituo vya Afya visikae na makusanyo ya pesa na badala yake zipelekwe bank.


Wilaya ya Sengerema ina jumla ya Vituo vya Afya 46 vinavyomilikiwa na Serikali Zahanati 41 na Vituo 5.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.