• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS Mwanza aipongeza Kamati ya Amani ya Mkoa huo kwa kuandaa Mafunzo ya Sensa

Posted on: June 28th, 2022

Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike ameipongeza Kamati ya Amani ya Mkoa kwa kuiunga mkono Serikali  katika kuhamasisha zoezi la Sensa ya Watu na Makazi na kutaka iendelee hivyo katika mambo mengine ya Kitaifa.

Akifungua mafunzo kuhusu Sensa inayowashirikisha Viongozi wa Dini kutoka Wilaya za Mkoa wa Mwanza,Ngusa amesema Wananchi wana kila sababu ya kushiriki zoezi hilo kwa Maendeleo ya Taifa letu.

"Mmefanya Jambo zuri kamati ya Amani ya Mkoa kutoa mafunzo haya, Sensa ni muhimu sana kwa Serikali kupanga mipango ya Maendeleo tuna imani Wananchi watahamasika kushiriki kuhesabiwa" amesema Samike

"Nawashauri pia kwenye nyumba zenu za ibada wahamasisheni waumini kwa kuweka mabango yenye ujumbe wa Sensa lengo likiwa wananchi washiriki kikamilifu" amesema Ngusa

Ngusa amesema wapo baadhi wenye uelewa mdogo au kuingia shaka  kuhusu Sensa lakini kwa kupeana elimu hii ni fursa nzuri ya kubadilishana uzoefu kati yenu Viongozi wa Dini na Serikali na hatimaye Wananchi watapata uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa Sensa na Makazi.

Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Mwanza Sheikh Hassan Kebeke amesema mafunzo hayo ni matokeo ya kuitikia wito wa Mhe Rais Samia Suluhu Hassan wa kuwataka Viongozi wa Dini kuhamasisha Sensa.


Naye Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Amani Askofu Charles Sekelwa amebainisha hata maandiko matakatifu yanatufundisha kuhusu Sensa hivyo wajibu wao kama Viongozi wa Dini kuendelea kuwaelimisha waumini wao.

Mafunzo hayo yanawashirikisha Viongozi wa Dini kutoka Wilaya zote za Mkoa wa Mwanza na yanatolewa na Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu Joachim Otaru.

Sensa ya Watu na Makazi itafanyika nchi nzima Agosti 23 mwaka huu kwa wale walio lala ndani ya mipaka wa Tanzania.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.