• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA ATOA RAI KWA WARATIBU TASAF KUTUMIA MFUMO WA MANUNUZI KWA UFANISI

Posted on: February 21st, 2024

RAS MWANZA ATOA RAI KWA WARATIBU TASAF KUTUMIA MFUMO WA MANUNUZI KWA UFANISI


*Aagiza kutatuliwa kwa changamoto zote ili Mfumo wa NEST utumike ipasavyo*


*Atoa wito kwa Maafisa hao kutoa taarifa za uaminifu kwa walengwa kwa wakati*


*Asema Mwanza imepokea zaidi ya Bilioni 91 kuanzia Julai 2015 kwa wanufaika*


*Ataka wafuatiliaji kuwa wazalendo katika kuwafikia walengwa na wanufaika*


*Asema zaidi ya miradi 174 ya zaidi ya Bilioni 33 imetekelezwa Mwanza*


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amewataka Waratibu na watendaji kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF) kuzingatia Sheria na Kanuni za Matumizi ya Mfumo wa Manunuzi (NEST) na Utoaji wa taarifa ili kuwahudumia walengwa kwa ufanisi.

Balandya amebainisha hayo mapema leo Februari 21, 2024 wakati akifungua Kikao kazi cha kujadili maendeleo ya Utekelezaji wa Mpango wa TASAF na Matumizi ya Mfumo wa Manunuzi (NEST) na Mfumo wa Taarifa wa TASAF kinachofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

"Mfumo wa Ununuzi na Mfumo wa Utoaji taarifa wa TASAFni muhimu sana katika Utekelezaji wa Mradi wa TASAF kwa ujumla wake katika kuhakikisha umasikini unaondoka kwa wananchi  kama ilivyokusudiwa na wafadhili wa mradi huo." Amesema Katibu Tawala.

Aidha, Katibu Tawala huyo amebainisha kuwa Mwanza imepokea zaidi ya Bilioni 91 kuanzia Julai 2015 kwa wanufaika 71,381 huku zaidi ya miradi 174 ya zaidi ya Bilioni 33 ikitekelezwa Mkoani humo tangia uzinduzi rasmi wa mradi huo Mkoani Mwanza mpaka sasa na kwamba fedha hizo ni nyingi zinahitaji uzalendo kwenye usimamizi.

Bi. Haika Shayo, Mkurugenzi wa Uratibu kutoka TASAF amesema wapo Mwanza katika kikao kazi cha kawaida cha kupitia utekelezaji wa shughuli za mradi  ili kuhakikisha mradi huo unafanyika kwa ufanisi na kujifunza matumizi ya Mfumo wa Ununuzi katika ngazi ya Halmashauri na Mfumo wa Taarifa wa TASAF.

"Hatuna budi kuwa na taarifa sahihi na za wakati kwa walengwa ili kuhakikisha wanaufurahia na unawahudumia kwa ufanisi hivyo baada ya kikao kazi hiki tunatarajia ufanisi mkubwa zaidi kwa watendaji wetu." Amesema Bi. Shayo, Mkurugenzi wa Uratibu TASAF.

Vilevile, amebainisha kuwepo kwa changamoto ya matumizi ya mfumo wa manunuzi hivyo ni imani yake kwamba kupitia mafunzo hayo ya siku 3 ya uwezeshaji  changamoto hiyo itatatuliwa  kwani wahusika wote ikiwemo Waratibu, Wahasibu, Maafisa Ufuatiliaji wa Mpango wa TASAF,  Maafisa Manunuzi  wamehusishwa katika mafunzo haya.

Monica Mahundi, Mratibu wa Mpango wa TASAF Mkoa wa Mwanza amebainisha kuwa jumla ya wanufaika 71,381 wamefikiwa huku Miradi 174 katika Sekta za Elimu, Afya na Miundombinu ya Barabara yenye zaidi ya Bilioni 33 zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.