• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA AZINDUA BODI YA USHAURI YA MWACHAS

Posted on: April 3rd, 2025

RAS MWANZA AZINDUA BODI YA USHAURI YA MWACHAS


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza  Ndg.Balandya Elikana leo Aprili 3,2025 amezindua rasmi Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi Mwanza (MWACHAS) huku akitoa wito kwa uongozi wa chuo na wadau wa elimu kushirikiana katika kuboresha sekta ya afya kupitia mafunzo bora kwa wanafunzi.

Akizungumza wakati wakati wa uzinduzi huo uliofanyika chuoni hapo eneo la Bugando wilayani Nyamagana, Balandya ameipongeza MWACHAS kwa hatua yake ya kuunda bodi imara ya ushauri akisisitiza kuwa taasisi za elimu zina jukumu kubwa la kuandaa wataalamu wa afya watakaosaidia kuboresha huduma za tiba nchini.

"Tunahitaji kuhakikisha kuwa vyuo vya afya vinakuwa na mifumo madhubuti ya kusimamia ubora wa elimu na mafunzo ili kuzalisha wahitimu wenye weledi wa hali ya juu,"Katibu Tawala

Aidha, ameitaka bodi hiyo kushirikiana na Serikali pamoja na wadau wengine ili kutatua changamoto zinazokabili chuo, hususan katika upatikanaji wa miundombinu bora.

 "Serikali iko tayari kushirikiana nanyi lakini ni lazima kuwe na mipango thabiti ya maendeleo ili MWACHAS iwe chuo bora kinachotoa mafunzo yenye viwango vya kimataifa".amesisitiza mtendaji huyo wa mkoa

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi hiyo Bw.Isaaka Ndasa amesisitiza kuwa jukumu kuu la bodi hiyo ni kuhakikisha MWACHAS inazidi kupiga hatua na kuwa miongoni mwa taasisi za elimu ya afya zinazoongoza nchini.

 "Tutahakikisha tunasimama imara ili kuboresha viwango vya elimu, kufuatilia mwenendo wa chuo na kuhakikisha kwamba chuo chetu kinaendelea kukua",Ndasa


Mwenyekiti huyo pia ametoa wito kwa wanachama wa bodi hiyo kufanya kazi kwa bidii na ushirikiano ili kutimiza malengo ya chuo.

Mkuu wa Chuo, Prof.Hyasinta Jaka ambaye pia ni Katibu wa Bodi hiyo ameiomba Serikali kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili chuo hicho hasa katika eneo la ujenzi wa Chuo katika eneo lililopo karibu na Hospitali ya Wilaya ya Ilemela Mwanza.

Aidha amesisitiza kuwa chuo kina dhamira ya kutoa elimu bora kwa wanafunzi wake, lakini kinahitaji msaada zaidi ili kuboresha vitendea kazi na kuongeza idadi ya wahadhiri wenye uzoefu.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na viongozi wa Serikali, wadau wa elimu, wahadhiri, na wanafunzi wa MWACHAS.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.