• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AAGIZA KUREJESHWA HALMASHAURI KAMPUNI YA MISUNGWI CO. LTD

Posted on: June 21st, 2023
  1. RC MAKALLA AAGIZA KUREJESHWA HALMASHAURI KAMPUNI YA MISUNGWI CO. LTD


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amemuagiza Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi na Idara ya Mipango kuhakikisha wanafanya Marekebisho ya Mapendekezo ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) ili kuhakikisha Kampuni ya Misungwi Company Ltd inamilikiwa na Halmashauri kwa asilimia 100.

Akizungumza kwa niaba yake leo tarehe 21 Juni, 2023 Katibu Tawala Mkoa Ndugu Balandya Elikana wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani Maalum la Kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Mwaka wa fedha 2021/22 amesema haiwezekani Kampuni ya Serikali ikaanzishwa na kuendeshwa kwa kukiuka taratibu za umiliki wa Makampuni ikiwemo Mkurugeni wa Halmashauri kuwa Mbia binafsi.

Vilevile, ameiagiza TAKUKURU ndani ya siku 30 kufanya uchunguzi ili kubaini uendeshwaji wa Kampuni hiyo iliyoanzishwa kwa hati ya Usajili Na 140457876 Novemba 21, 2019 ikiwa na Mali za TZS 35,547,983 na fedha Taslimu TZS 24,547,983 na thamani ya Mashine TZS 11,000,000 huku ikiwa na udhaifu kwenye Muundo na Usimamizi na kukosekana kwa gawio la moja kwa moja kwa Halmashauri hiyo.

Aidha, Elikana ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kupata Hati safi na amewataka kuwa na Mwenendo wa kushughulikia Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu kwa haraka ili kujihakikishia wanaendelea kupata Hati safi na kwamba hilo linawezekana endapo watafuata taratibu na Kanuni za Mapato na matumizi ya  Fedha za umma.

Akiwasilisha taarifa kwa niaba ya Mkurugenzi, Mweke Hazina wa Halmashauri hiyo Ngugu Joseph Mazito amesema pamoja na kupata Hati Safi Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali katika mwaka 2021/22 alitoa hoja 16 ambazo zilitakiwa kujibiwa na kuwasilisha majibu kwa ajili ya uhakiki

"Hadi kufikia tarehe ya kikao hiki majibu ya hoja hizo yaliwasilishwa na kuhakikiwa na hoja zilizotekelezwa na kufungwa ni 12 sawa na asilimia 75 huku hoja zinazoendelea kutekelezwa zikiwa ni 4 sawa na Asilimia 25 ambapo jitihada zinaendendelea kuhakikisha zinajibiwa." ameeleza Mwekahazina.

Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Nje Mkoa wa Mwanza, Waziri Shaban ameipogeza Halmashauri ya wilaya ya Misungwi kwa kupata Hati safi na akabainisha kuwa wamekua na mwenendo wa kupata Hati Safi kwa zaidi ya miaka 3 mfululizo na ametoa wito kwa watendaji kuheshimu taratibu za fedha.

"Tunawapongeza Halmashauri ya wilaya ya Misungwi kwani kwa Mwaka wa fedha 2021/22 Halmashauri hiyo ilikaguliwa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na imepata Hati safi huku wakiwa na Agizo moja tu la LAAC ambalo hawajalitekeleza na kuonesha juhudi za kuitekeleza" amesema Ndugu  Waziri Shaban.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.