• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AHIMIZA KUHARAKISHWA MAENDELEO YA WANANCHI MAGU

Posted on: June 27th, 2023

RC MAKALLA AHIMIZA KUHARAKISHWA MAENDELEO YA WANANCHI MAGU


*Aagiza miradi ya maendeleo ikamilike kwa wakati, ubora na ilingane na thamani ya fedha*


*Ataka iwepo ratiba maalum ya ufuatiliaji wa Miradi*


*Aipongeza Halmashauri ya Magu kwa kuwa na hoja chache*



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA. Amos Makalla ameitaka Menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Magu kuisimamia miradi ya maendeleo ili kutimiza matarajio ya wananchi.


Mhe. CPA. Makalla amesema hayo leo Juni 27, 2023 wakati wa Mkutano wake wa mwisho wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu kwa ajili ya kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za Mwaka 2021/22  zinazoishi Tarehe 30 Juni 2022.

" Tukasimamie miradi ya maendeleo ibadilike kutokukamilika kwa miradi hiyo tunafifisha imani ya wananchi tutumie matarajio ya wananchi kama tulivyo ahidi kuhakikisha inakamilika kwa kiwango kinachotakiwa kwa thamani ya fedha  kwa kufanya hivyo tutaendelea kuwatendea haki wananchi wetu," RC Makalla.

"Wekeni ratiba ya kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa menejimenti tekelezeni yale ambayo yanaelekezwa katika ilani Chama cha Mapinduzi CCM, Madiwani wamekamilisha wajibu wao ni kazi ya menejimenti yale mliyoyaahidi katika vikao vya kujibu hoja kuyatekeleza kila mmoja katika eneo lake.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa ameitaka Halmashauri hiyo kuendelea kutoa ushirikiano kwa ofisi ya CAG katika kila hatua ili ukaguzi ujao kusiwe na hoja pia kumtumia vizuri mkaguzi wa ndani katika kuhakikisha wanazimaliza hoja.

Vilevile RC. Makalla ametoa rai kwa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Kufanyia kazi taarifa za mkaguzi wa ndani ili kupunguza hoja na Menejimenti kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wakaguzi ili waweze kupata hati safi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu Mhe. Mpandalume Simon amesema wanakwenda kutufanyia kazi mpango kazi ambao utaenda kujibu hoja zote za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Naye, Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Nje wa Mkoa wa Mwanza Waziri Shabani kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amesema anatambua ushirikiano alioupata kutoka kwa wafanyakazi na menejimenti ya Halmashauri ya wilaya ya magu wakati wa ukaguzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.