• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AHOJI ONGEZEKO LA GHARAMA SHILINGI BILIONI 11 KUPEWA KAMPUNII YA EMIRATES BUILDERS LTD MRADI WA MAJI USAGARA

Posted on: November 7th, 2023

RC MAKALLA AHOJI ONGEZEKO LA GHARAMA SHILINGI BILIONI 11 KUPEWA  KAMPUNII YA EMIRATES BUILDERS LTD MRADI WA MAJI USAGARA


*Aagiza TAKUKURU kuchunguza mkandarasi aliyeshinda tenda ya awali kwa Shilingi bilioni 21 kukataliwa na kupewa Kampuni ya EMIRATES kwa shilingi Bilioni 32*


*Ataka taarifa ya Uchunguzi huo ikamilike ndani ya siku 14*


*Awataka RUWASA Makao Makuu kutoa ushirikiano kwani wao ndio waliompa mkandarasi EMIRATES Ltd kwa gharama kubwa*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Makalla ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kuchunguza sababu za mkandarasi aliyeshinda tenda ya awali kwa Shilingi bilioni 21 kukataliwa na kupewa Kampuni ya EMIRATES kwa Shilingi Bilioni 32 kwenye Mradi wa Maji Ukiriguru wilayani Misungwi.

Makalla ametoa agizo hilo mapema leo Novemba 07, 2023 wakati wa ziara yake wilayani Misungwi (Ukiriguru-Usagara) wakati akikagua Mradi Mkubwa wa Maji unaokwenda kunufaisha zaidi ya wananchi elfu 85 kwenye maeneo mbalimbali huku ukitarajiwa kuwa na Matanki Makubwa 4 yenye ujazo wa Lita Milioni 6.5

Mhe. Makalla amehoji ni kwanini Mkandarasi Emirates Builders Limited mwenye gharama za juu za ujenzi kwa ongezeko la zaidi ya Bilioni 11 tofauti na Mkandarasi aliyeshinda awali apewe kazi hiyo na kwamba imepata hofu ya Ukiukwaji wa sheria na taratibu za Zabuni na ndipo akaagiza uchunguzi huku akiwataka kutumia siku 14 kukamilisha zoezi hilo na taarifa aipate.

Aidha, ametoa wito kwa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Makao Makuu kutoa ushirikiano kwenye uchunguzi huo kwani wamesimamia taratibu za kumpata mkandarasi huyo aliyepatikana kwa gharama za juu tofauti na makampuni mengine yaliyohitaji kazi hiyo kwa Bilioni 19 na 21 lakini wakaamua kumpatia mwenye gharama za juu.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwataka RUWASA kusimamia vizuri mradi huo ukamilike ndani ya muda uliopangwa wa miaka miwili hadi februari 2025 na amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kujenga mradi huo kwani hadi sasa zaidi ya Bilioni 5 zimeshatolewa na mradi umefikia asilimia 12 ya utekelezaji wake.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.