• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AKEMEA HUJUMA KWENYE MIRADI INAYOTEKELEZWA MWANZA

Posted on: July 19th, 2023

RC MAKALLA AKEMEA HUJUMA KWENYE MIRADI INAYOTEKELEZWA MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amesema hatokuwa tayari kuona baadhi ya watu wanazorotesha miradi mbalimbali inayotekelezwa Mkoani humo na badala yake hatua kali za kisheria watachukuliwa.

Akizungumza leo kwa niaba yake wakati wa hafla fupi ya utiaji saini wa mikataba miwili ya ujenzi wa Tanki la maji Nyamazugo na upanuzi wa mtandao wa bomba Km 73  Wilayani Sengerema,Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza,Ndg.Balandya Elikana amesema wananchi wanapaswa kutanguliza uzalendo kwa kuilinda miradi hiyo kwani ipo kwa faida yao.

"Hizi hujuma hatuwezi kuzifumbia macho,miradi inaletwa kwetu ili irahisishe maendeleo,unapofanyika wizi ni dhahiri miradi hiyo haiwezi kumalizika kwa wakati na hatimaye malengo yaliyo kusudiwa kushindwa kumalizika kwa wakati,"amesisitiza Mtendaji huyo wa Mkoa.

Amesema mradi anaoshuhudia ukitiwa saini tayari kwa ujenzi wa Tanki la maji la ujazo wa lita 5,000,000 wenye thamani ya Shs bilioni 2.7 na upanuzi wa mtandao wa bomba wa Km 73 wa thamani ya Shs milioni 937,673,750,hizo ni fedha nyingi zinazotolewa na Serikali kwa kuthamini maendeleo ya wananchi hivyo ni wajibu kwa kila mmoja kuunga mkono jitihada hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sengerema,Mhe.Senyi Ngaga amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu kwa kuonesha kwa vitendo jitihada za kuwaletea maendeleo wananchi kwa miradi mbalimbali kuanzia sekta ya afya,elimu,na maji.

"Nina kila sababu ya kuishukuru Serikali hii ya awamu ya sita kwa hizi jitihada za kumtua mama ndoo kichwani,kwa miaka ya nyuma wananchi wangu wa Jimbo la Sengerema wametaabika sana na upatikanaji wa huduma hii ya maji,"Mhe Hamis Tabasamu,Mbunge wa Sengerema CCM

"Mradi huu wa Tanki la maji utakapo kamilika utaweza kuhudumia wakazi wa Sengerema wapatao 166,500 hivyo kuzidi kwenda na malengo ya Serikali ya kufikisha huduma ya maji kwa asilimia 95 mjini na asilimia 85 vijijini ifikapo mwaka 2025,"Mhandisi Sadala Hamisi,Mkurugenzi Mtendaji Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mjini Sengerema(SEUWASA)

Mradi wa ujenzi wa Tanki la maji utatekelwzwa na Mkandarasi NANGH'WARE MHANDI LIMITEDH na ule wa upanuzi wa mtandao wa bomba Km 73 wakandarasi  ni 3 Zabuni ya bomba ni LAKE PIPES LIMITED,Zabuni ya viungio vya mabomba ni KAKENGI INDUSTRY AND GENERAL SUPPLY na Zabuni ya uchimbaji muhusika ni LOCAL FUNDI.





Miradi hiyo itatekelezwa kwa muda wa miezi 6 kuanzia Agosti mwaka huu hadi January 2024.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.