• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AKIPONGEZA KIWANDA CHA UCHENJUAJI NA USAFISHAJI WA MADINI

Posted on: August 10th, 2023

RC MAKALLA AKIPONGEZA KIWANDA CHA UCHENJUAJI NA USAFISHAJI WA MADINI


*Aridhishwa na Biashara ya Madini katika Soko la Madini Mwanza*


*Aahidi Mkutano mkubwa wa wadau wa Madini*


*Asema Mgodi mkubwa wa Pili Tanzania wa Nyanzaga kuanza Mwezi septemba wilayani Sengerema*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla amekipongeza kiwanda cha uchenjuwaji na usafishaji madini kwa kufanya shughuli zake kwa Teknolojia ya juu hali inayofanya dhahabu ya kutoka Tanzania kuwa na viwango  bora kwenye soko la Dunia.

Akizungumza leo na wanunuzi wa madini na uongozi wa kiwanda cha kusafisha madini wakati wa ziara fupi aliyoifanya kiwanda hapo Wilayani Ilemela, Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha thamani ya uwekezaji huo wa Bilioni 16.5 umekwenda pamoja na ubora wa shughuli husika  na Serikali kuwa na uhakika wa mapato.

"Nimefika hapa nimejionea kazi zinavyofanyika na taarifa za kiwanda hiki hakika nawapa pongezi,nitawatembelea wachimbaji Kwimba na Misungwi kuwapa hii taarifa namna Serikali ilivyoweka mazingira mazuri kwao na waitumie fursa hii ",CPA Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla ameridhishwa na biashara ya madini katika soko la bidhaa hiyo mara baada ya kuwasikiliza na kujionea shughuli zao na kuwaahidi Serikali ya Mkoa kuwasaidia kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazowakabili ili wafanye shughuli zao katika mazingira rafiki na kuendelea kuwawekea mazingira mazuri wawekezaji watakaojitikeza.

"Nimezungumza na Afisa Madini wa Mkoa Mhandisi Nyaisara Mgaya aandae taarifa zote muhimu kuhusiana na shughuli za Madini ili wadau wapate ufahamu wa kutosha wakati wa mkutano mkubwa nitakao itisha",amesisitiza Makalla.

"Nimezungumza na mwekezaji wa mgodi wa Nyanzaga wenye thamani ya Dola milioni 474 ambao utaanza shughuli zake hivi karibuni,watumie kikamilifu fursa zilizopo kiwandani hapa na siyo kwenda sehemu nyingine Mhe.Makalla

"Kiwanda hiki mhe.Mkuu wa Mkoa kina mitambo ya kisasa ya kusafisha madini na kuifanya kuwa kwenye ubora wa kimataifa na hivi sasa tunatarajia Benki Kuu ya Tanzania kuja kuyanunua Madini hapa kama sheria inavyoelekeza,"Deus Magala,Meneja Rasilimali Watu Kampuni ya Uchimbaji Madini,STAMICO.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa sisi kama wadau wa Madini Bado tuna changamoto za hapa na pale hasa upungufu wa malighafi ambao unatufanya tutumie muda mwingi kusubiri na wakati mwingine kutufanya kutoka na kwenda sehemu nyingine kutafuta Madini,"William Kulindwa,Mwenyekiti soko la madini Mwanza.

Kiwanda cha kusafisha madini kilichoanza shughuli zake mwaka 2021 baada ya kuzinduliwa na Rais Dkt.Samia Suluhu,kinafanya kazi kwa ubia kati ya Serikali yenye asilimia 25 na mwekezaji kutoka Sudan mwenye asilimia 75


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.