• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AONGOZA HARAMBEE YA KUICHANGIA PAMBA JIJI FC, ZAIDI YA MILIONI 177 ZAPATIKANA

Posted on: February 12th, 2024

RC MAKALLA AONGOZA HARAMBEE YA KUICHANGIA PAMBA JIJI FC, ZAIDI YA MILIONI 177 ZAPATIKANA


*Awashukuru wachangiaji kwa kufanikisha harambee*


*Ahimiza kuipa nguvu ya kiuchumi Pamba FC kwa kununua jezi kwa wingi*


*Awahakikishia wana Mwanza fedha zitakuwa salama*


*Abainisha Mkakati wa kuipandisha timu hiyo Ligi kuu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Februari 11, 2024 amewaongoza Wana Mwanza na wadau wa michezo katika harambee ya kuichangia timu ya soka ya Pamba Jiji FC na kufanikisha kukusanya jumla ya Shilongi milioni 177.3

Harambee hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mwanza Hotel michango hiyo imetoka kwa watu, taasisi mbalimbali za Serikali na watu binafsi wameitikia kwa wingi zoezi hilo lenye lengo la kuipa nguvu Pamba FC katika michezo yake ya Ligi ya Championship ili ipande kwenda Ligi kuu.

Katika hotuba yake ya kuwashukuru waliofanikisha harambee hiyo Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mlezi wa timu hiyo maarufu kama TP Lindanda amebainisha kuwa kupanda Ligi kuu siyo lele mama bali ni lazima kuwe na mikakati ya uhakika wa kifedha ambayo ndiyo chanzo cha mafanikio.

"Nilipoingia rasmi kama Mkuu wa Mkoa huu niliichunguza Pamba FC na kubaini inahitaji haraka nguvu ya kifedha, wameingia ndugu zetu wa NetSports hatuna budi kununua jezi kwa wingi ili kuzidi kuimarisha kiuchumi timu hii", CPA Makalla

Hotuba hiyo ya Mkuu wa Mkoa iliwaongezea hamasa washiriki wa harambee hiyo na kuzinunua kwa wingi jezi za Pamba Jiji wakiongizwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mwanza Mhe. Michael Masanja.

"Ndugu mgeni rasmi Mkuu wetu wa Mkoa hizi jitihada zako sisi kama viongozi wa soka Mkoa zinazidi kutupa ari kuwa mstari wa mbele kuipigania Pamba Jiji FC ili ifike malengo ya kupanda Ligi kuu msimu ujao," Vedasto Lugano M/kiti MZFA.

Meya wa Jiji la Mwanza ambaye ni wamiliki wa Pamba Jiji FC Mhe. Costantine Sima amebainisha watahakikisha nguvu hiyo ya wadau haipotei bure bali utakuja na matokeo chanya ambayo ni kucheza Ligi kuu msimu ujao.

Fedha hizo zilizotokana na harambee ni pamoja na michango taslimu ambayo ni zaidi ya Shilingi Milioni 28 na ahadi zaidi ya Shilingi milioni 100.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.