• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ATEMBELEA MIRADI, AHIMIZA IKAMILIKE KWA WAKATI

Posted on: June 16th, 2023

RC MAKALLA ATEMBELEA MIRADI, AHIMIZA IKAMILIKE KWA WAKATI


*Aitaka Halmshauri ya Jiji kuweka mazingira ya muingiliano wa watu soko la Wafanyabiashara wadogo*


*Awakumbusha kuheshimu taratibu zilizowekwa na Serikali za kutengewa maeneo maalum*


*Stendi kuu ya Mabasi Nyegezi kufunguliwa na Rais Samia*


*Aahidi kusimamia Mradi wa Maji ukamilike kwa wakati wananchi waondokane na kero ya maji*



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Juni 16, 2023 amekagua Miradi  ya Soko la Machinga la MchafuKoga, Stendi kuu ya mabasi Nyegezi na mradi wa Maji Butimba Wilayani Nyamagana na kutaka miradi hiyo ikamilike kwa wakati ili kuleta tija ya wananchi.

Akianzia soko la Mchafu Koga linalojengwa kwa gharama ya zaidi ya Shs. bilioni 1.4 ameutaka uongozi wa Jiji la Mwanza kuhakikisha wanafanya shughuli zao katika mazingira rafiki yenye muingiliano wa watu ili wajihakikishie wateja.

"Nimesikia taarifa yenu ya ujenzi wa soko hili, lakini mtambue siyo tu kujenga soko zuri bali mzingatie kufikiwa na wananchi kiurahisi ikiwemo mabasi kupita maeneo haya ili watembea kwa miguu wazione bidhaa kirahisi," CPA Makalla.

Amewakumbusha pia wafanyabiashara hao ndogo ndogo kuendelea kuheshimu taratibu zilizowekwa na Serikali za kutengewa maeneo yao maalum na siyo kukimbilia kupanga bidhaa zao barabarani.

Akisoma taarifa ya mradi wa ujenzi wa soko kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Edward Mwamotela amesema ili kuendeleza ujenzi wa Block B na C Halamashauri imepokea Shilingi Bilioni 9 kwa mwaka wa fedha 2022-2023 kutoka mradi wa Green and Smart Cities na kwa mwaka wa fedha ujao 2023-2024 imetengwa bajeti ya shilingi Bilioni 1 kutoka mapato ya ndani.

"Uongozi wa Wilaya na Mkurugenzi kaeni na wadau wote waliopo hapa stendi ili mzisikilize changamoto zilizopo hapa na mzishughulikie na msikilize ushauri wao juu ya namna ya kuendesha standi ili kutoka na mapendekezo mazuri," amesema Mhe. CPA. Makalla.

Amesema wakati Stendi hiyo ya mabasi iliyokamilika kwa asilimia 100 na kuwa katika majaribio kero zote zitatuliwe na atamuomba Rais Mhe.Dkt.Samia Suluhu kuja kuifungua rasmi.

"Ujenzi wa stendi ya Nyegezi umekamilika kwa asilimia 99.5 na kazi zilizobaki ni kufunga Mageti na  Stendi imeanza kufanya kazi tarehe 5, Juni 2023, Stendi ya Nyegezi ina eneo la kuegeshea mabasi 120 na magari madogo 80 kwa wakati mmoja,"amesema  Edward Mwatomola, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji.

Akikagua mradi wa maji wa Butimba uliogharimu Shs. bilioni 69 na kutarajiwa kuukamilishwa na kukabidhi kwa Serikali Julai 30 mwaka huu na Mkandarasi SOGEA SATTON kutoka Ufaransa, Makalla amesema atausimamia kidete kuhakikisha makubaliano ya makabidhiano yanafanyika kama ilivyopangwa ili wananchi waondokane na tatizo la maji.

Halamashauri ya Jiji la  Mwanza ni miongoni mwa Halmashauri ambazo zinatekeleza miradi ya kimkakati ambayo inalenga kuziwezesha Halmashauri nchini  kuongeza mapato na kupunguza utegemezi kwa Serikali kuu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.