• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AUKABIDHI RASMI MWENGE WA UHURU SIMIYU,MIRADI YENYE KASORO AHAIDI KUIFANYIA KAZI HARAKA

Posted on: July 21st, 2023

RC MAKALLA AUKABIDHI RASMI MWENGE WA UHURU SIMIYU,MIRADI YENYE KASORO AHAIDI KUIFANYIA KAZI HARAKA


*Awapongeza wakimbiza Mwenge Kitaifa kwa ukakamavu na uwezo wa kukagua miradi


*Ajivunia ubora wa miradi yenye tija kwa wananchi iliyozinduliwa na Mwenge wa Kitaifa


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Makalla leo ameukabidhi rasmi Mwenge wa Uhuru kwa Mkoa wa Simiyu na kujivunia miradi yote iliyozinduliwa na Mwenge huo yenye thamani ya Shs bilioni 21 itakuwa na tija kwa wananchi.

Akimkabidhi Mwenge huo kwenye viwanja vya shule ya msingi Kiloleli Wilayani Busega, kwa mwenzake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Dkt.Yahaya Nawanda,CPA Makalla amebainisha miradi michache iliyobainika na kasoro atahakikisha inafanyiwa kazi na kumpa taarifa kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Abdalla Shaib Kaim kabla ya Julai 31,2023

"Ndugu Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa,miradi ambayo imeonesha utata nakuahidi kutumia vyombo husika kama Takukuru ili kubaini tatizo na hatua za kisheria kuchukuliwa,"amesisitiza Mhe.Makalla.

Ameongeza kuwa Mwenge wa Uhuru umekimbizwa kwenye Wilaya zote 7 zenye jumla ya Halmashauri 8 kwa utulivu na usalama na wanajivunia miradi isiyopungua 50 imeonesha kuwa kwenye ubora na tija kwa wananchi wa Mwanza.

"Asanteni sana ndugu zangu wa Mwanza kwa ukarimu na mapokezi mazuri tangu tulipoingia Mkoani hapa Julai 13,2023,rai yangu kwa viongozi tuendelee kuchapa kazi na kuisimamia vizuri miradi yote inayotekelezwa Mkoani hapa yenye malengo ya kumletea maendeleo mwananchi,tuwe makini kubaini changamoto na kuzipatia ufumbuzi haraka na siyo hadi viongozi wa Kitaifa waingilie kati," amesema Abdallah Shaib Kaim,Kiongozi wa Kitaifa mbio za Mwenge wa Uhuru.

Kauli mbiu ya mbio za Mwenge wa Uhuru inasema "Tunza Mazingira,Okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa viumbe hai kwa Ustawi wa Taifa".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.