• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AVALIA NJUGA KILIMO CHA PAMBA KUKUTANA NA MAAFISA UGANI WOTE KUPANGA MKAKATI WENYE TIJA

Posted on: December 8th, 2023

RC MAKALLA AVALIA NJUGA KILIMO CHA PAMBA KUKUTANA NA MAAFISA UGANI WOTE KUPANGA MKAKATI WENYE TIJA


 *Asema Pamba ndiyo zao la kuinua uchumi wa mkulima na Taifa*


*Kukutana na uongozi wa ATCL kuweka mkakati wa ndege ya mizigo iwanufaishe wafanyabiashara*


*Atangaza mpango wa kuinua ufaulu wa wanafunzi na kukomesha utoro shuleni*


*Maafisa ardhi awataka kutokaa ofisini na badala yake kwenda kutatua migigoro ya ardhi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA Amos Makalla leo Disemba 8, 2023 amefungua kikao cha bodi ya ushauri wa Mkoa na kuweka bayana mikakati mbalimbali ya kimaendeleo likiwemo usimamizi wenye tija wa zao la Pamba kwa kukutana maafisa Ugani wote hivi karibuni.

Akizungumza na wajumbe wa kikao hicho kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Makalla amebainisha hakuna sababu ya zao la Pamba kuzorota wakati Serikali imeboresha kwa kiwango kikubwa sekta ya kilimo nchini.


"Wiki ijayo nitakutana na Maafisa Ugani wote kuanzia ngazi ya kata hadi juu, lengo tuone namna ya kulifanya zao hili liwe na tija kiuchumi kwa mkulima na Taifa kwa ujumla" CPA Makalla

Amesema Serikali imeweka mazingira rafiki kwa mkulima kwa kumpunguzia gharama za Pembejeo na kuboresha mbegu bora, hivyo ni wakati mwafaka kwa Mwanza kurudusha uzalishaji na kutoa Pamba itakayokidhi soko la kimataifa.


Kuhusu miradi ya maendeleo ya kimkakati Mkuu huyo wa Mkoa amewataka viongozi wote kutanguliza maslahi ya Taifa kwa kufanya usimamizi mzuri na hatimaye iwe na tija kwa manufaa ya wananchi.

"Rais wetu ametoa Shs bilioni 30 kwa ajili ya ukarabati wa uwanja wa ndege,wiki ijayo nikiwa na RAS tutakwenda kuonana na uongozi wa ATCL kwa lengo la ndege mpya ya mizigo iwanufaishe wafanyabiashara wa minofu ya samaki,nyama na mingineyo na hii ni baada ya kuvitembelea viwanda vyao na kusikia kilio chao katika usafirishaji,"amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa wakati anazungumza na wajumbe wa bodi ya ushauri wa mkoa


Kwa upande wa migigoro ya ardhi CPA Makalla amebainisha baada ya kuzunguka Wilaya zote za mkoa wa Mwanza amebaini kero nyingi zinatokana na watumishi kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo

"Kuna kiwanja kipo maeneo ya Liberty nimeamuru Halmashauri ya Jiji wamrudishie muhusika halali baada ya kubaini kuwepo na dhuluma ya waziwazi huu ni mfano mmojawapo ambayo ni mbaya kwa watendaji wetu,narudia kusema tukomeshe tatizo hili,"Mkuu wa Mkoa


Aidha CPA Mkalla yupo mbioni pia kukutana na Maafisa elimu wote kuweka kipaumbele cha kiwango cha ufaulu na kukomesha utoro shuleni.

Awali akitoa hotuba fupi,Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Mhe.Michael Lushinge amesema kikao cha bodi ya ushauri wa mkoa ndiyo dira ya Mkoa kimaendeleo hivyo kuwataka wajumbe wote kwenda kuifanyia kazi mipango yote itakayowekwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.