• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO WAANDISHI WA HABARI MWANZA

Posted on: February 23rd, 2024

RC MAKALLA AWAHAKIKISHIA USHIRIKIANO WAANDISHI WA HABARI MWANZA


*Amewashukuru Waandishi kwa kutumia vema kalamu zao kuunganisha jamii*


*Aelekeza Taasisi zote Mwanza kutoa ushirikiano kwa wanahabari*


*Awaasa wanahabari kuandika kutoka kwenye vyanzo vya uhakika na ukweli*


*Abainisha ujenzi wa Jengo la Abiria la kisasa Airport Mwanza kuwa Kimataifa*


*Aahidi usaidizi  wa Pikipiki 2 na kuongoza Harambee ya ujenzi wa ofisi*


*Awasihi kutangaza miradi ya kimkakati na timu za Mwanza kucheza Ligi kuu*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema Ofisi yake itaendelea kushirikiana na waandishi wa habari kwenye kuhabarisha umma na kuhakikisha jamii inapata taarifa sahihi kwa wakati na kwa uhakika.


Makalla amesema hayo leo Februari 23, 2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari wa Mkoa huo kupitia chama chao (MPC)  katika kikao kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Makalla ametumia wasaa huo kubainisha furaha yake kwa waandishi wa habari hao kwani wamekua kiungo cha kuwafikia wananchi na ameomba umoja udumishwe zaidi kwenye ofisi mbalimbali ili kuifanya Mwanza kukua zaidi kiuchumi na maendeleo ya huduma za Jamii.


Aidha, amebainisha mpango wa Serikali wa kuboresha uwanja wa Ndege wa Mwanza kuwa wa Kimataifa hususani ujenzi wa Jengo la abiria la kisasa litakaloanza kujengwa ndani ya wiki mbili zijazo na kwamba utasaidia kukuza utalii mkoani humo.

Mwenyekiti wa MPC Edwin Soko ametumia wasaa huo kuwasilisha ombi kwa Mkuu wa Mkoa kuwa mgeni rasmi kwenye Harambee ya Kuchangia fedha za ujenzi wa Ofisi ya Chama hicho itakayofanyika siku za usoni.

Aidha, Soko amebainisha kuwa waandishi wa habari mkoani humo wapo kwa ajili ya kuhabarisha umma na kusaidia kupatikana kwa majawabu ya changamoto mbalimbi kwa jamii jambo ambalo wanafanya kwa weledi na kuzingatia maadili ya uandishi.

"Tunafanya kazi zetu kwa kuzingatia weledi na maadili hususani kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika mwaka huu pamoja na Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani wa Mwaka 2025" Amesema Mwenyekiti Soko.


Vilevile, ametumia wasaa huo kuziomba taasisi na mamlaka zote za Serikali Mkoani humo kuhakikisha wanazingatia usalama wa waandishi wa habari wakati wote wanapotumikia shughuli za uhabarishaji wa umma na kutowazungusha waandishi mara wanapohitaji taarifa.

Katika kuhakikisha wanakua na Ofisi yao na kuondokana na gharama za kupanga,  Soko ametoa rai kwa Mkuu wa Mkoa kuwasaidia waandishi wa Habari kwenye upatikanaji wa vitendea kazi mbalimbali vya Studio na vinginevyo pale ambapo Makalla ameridhia na kuahidi kuwanunulia Pikipiki 2 siku za usoni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.