• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA MWATEX KUWA WABUNIFU KUKABILI USHINDANI SOKO LA NGUO

Posted on: December 5th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA MWATEX KUWA WABUNIFU KUKABILI USHINDANI SOKO LA NGUO


*Awataka kuendana na soko la kisasa kwa kuwa wabunifu na wenye mikakati dhahiri ya kuinuka kibiashara*


*Awaagiza TANESCO na MWAUWASA kuwa na ratiba ya huduma inayofahamika kwa wateja*


*Atoa rai kwa kitengo cha biashara kutangaza kiwanda hicho ili kupata malighafi*


*Awaahidi kushirikiana nao kuboresha huduma katika kuendelea kufanya uzalishaji*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka wamiliki wa kiwanda cha uzalishaji nguo MWATEX 2001 LTD kuzalisha bidhaa nzuri na bora zinazokidhi soko la sasa kwenye jamii ili kujihakikishia katika eneo hilo

Mhe. Makalla ametoa wito huo mapema leo Disemba 05, 2023 alipofanya ziara kwenye kiwanda hicho kilichopo Nyakato na kubaini kushuka kwenye uzalishaji hadi Mita laki 5 kutoka Milioni 1 kwa mwaka  pamoja na uwepo wa malighafi hususani pamba mkoani humo.


Amesema, pamoja na changamoto zingine ni lazima kiwanda hicho kiwe na mkakati wa mipango ya muda mfupi na mrefu katika kuzalisha bidhaa bora na kuhakikisha wanayafikia malengo waliyoyapanga ya uzalishaji aidha wa kanga, shuka, mifuko na vitenge.

"Lengo la Serikali kubinafsisha viwanda hivi ni kupata tija hivyo ni lazima muongeze ubunifu ili kuyafikia malengo ya Serikali ya kuona vinazalisha na siyo kujificha kwenye visingizio mbalimbali" Mkuu wa Mkoa.


Vilevile, ametoa rai kwa kiwanda hicho kuboresha kitengo cha biashara ili kutangaza bidhaa zao huku Serikali ikiendelea kushirikiana nao kwenye kuboresha huduma za nishati ya maji na umeme.

Aidha, amewataka TANESCO na MWAUWASA kuwa na ratiba inayofahamika ya mgao wa huduma zao ili wenye viwanda waweze kujipanga kwenye uzalishaji kwani wanapokata bila taarifa wanawasababishia kupata hasara.


Katika kufafanua suala la nishati ya Umeme, Meneja wa TANESCO Kanda ya Nyakato Mhandisi Jackson Peter amesema matatizo ya kukatika kwa umeme yanakwenda kuisha siku za usoni lakini wataboresha utoaji wa taarifa kwa wakati.

Awali Bi. Mariam Msangi, Afisa Masoko wa kiwanda hicho alibainisha changamoto kadhaa zikiwarudisha nyuma kama uwepo wa nguo za mitumba na jamii kuacha kutumia mavazi ya asili, kukatika kwa maji na umeme pamoja na bei kubwa wanazotozwa na watoa huduma hizo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.