• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA WANACHAMA WA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA NYANZA KUWA WAZALENDO NA KUJENGA USHIRIKA IMARA

Posted on: March 27th, 2024

RC MAKALLA AWATAKA WANACHAMA WA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA NYANZA KUWA WAZALENDO NA KUJENGA USHIRIKA IMARA


*Abainisha kurejeshwa kwa Akaunti Maalum (ESROW ACCOUNT) ya Chama Kikuu cha Ushirika NYANZA*


*Ataka kutumika vizuri kwa Akaunti hiyo katika kufufua Ushirika na kuleta tija*


*Ataka Chama kujipanga kushindana katika Soko na sio kukopa Wakulima*


*Awataka kuwa na mkakati wa kufufua viwanda vya kuchaka pamba*


*Awataka kusimamia upatikanaji na ugawaji wa pembejeo za Kilimo kwa wakati*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amewataka Chama kikuu cha Ushirika Nyanza kulinda Mali kwa uzalendo na kuwa na hatimiliki ili zisipotee badala yake ziendelezwe ili zizalishe Mapato na kuwa na Chama imara chenye Ushindani sokoni.

Mhe. Makalla ametoa neno hilo mapema leo Machi 27, 2024 wakati akifungua Kikao cha Siku moja cha Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Chama Kikuu cha Ushirika Nyanza (NCU- Nyanza Cooperative Union) kilichofanyika kwenye chuo cha Ualimu Butimba.

Amesema, katika kuimarisha Ushirika ni lazima kila mmoja kwenye umoja huo awe mzalendo katika kulinda mali na vitega uchumi za chama hicho kama Mashamba, Magari, Maghala, Nyumba, Viwanda n.k ili visaidie kukuza ushindani na kupanua biashara ili zisaidie kukuza uchumi wa chama hicho.

Aidha, amewataka kuhakikisha wanaboresha mnyororo wa thamani wa zao la Pamba kwa kufufua viwanda vya kuchambua pamba kwani kwa kufanya hivyo wataongeza thamani ya zao hilo, uhakika wa soko na kipato kwa wanachama wake na sio kukopa mazao kwa wakulima na baadae kutafuta masoko.

Vilevile, amewataka wanaushirika kusimamia upatikanaji na ugawaji wa pembejeo za Kilimo cha Pamba kwa wakati kwa wanachama wake, pia akawaagiza Maafisa Ugani kujiridhisha na takwimu za Mahitaji ya Pembejeo za wakulima wa pamba ili kuwezesha kuwa na takwimu sahihi za mahitaji ya pembejeo hizo kwa wakulima.

"Tume ya Maendeleo ya Ushirika (TCDC) imeanza kutumia mfumo wa TEHAMA, tunataka kuhakikisha wanachama wote wanajisajiri kwa 100% na kuzingatia matumizi ya miongozo 15 ya biashara ili kuendana kiushindani." Amesema Gabriel Mwita, Mwakilishi wa Mrajis wa Vyama vya Ushirika Nchini.

Vilevile, Mwakilishi huyo wa Mrajis amezungumzia uwekezaji unaotarajiwa kuanza rasmi mwezi Mei mwaka huu ambao utawafanya washirika kuwa na asilimia 51 za hisa ili waweze kuimiliki benki ya Ushirika na kwamba kwenye vyama vya ushirika kunakua na SACCOS ili kuinua mitaji ya wanachama.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.