• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AWATAKA WATENDAJI WA KATA KUTENGA SIKU MOJA NDANI YA WIKI KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Posted on: October 19th, 2023

RC MAKALLA AWATAKA WATENDAJI WA KATA KUTENGA SIKU MOJA NDANI YA WIKI KUSIKILIZA NA KUTATUA KERO ZA WANANCHI


*Awataka kuwajibikwa kwa wananchi kwani ndio Dira ya Rais Samia*


*Aziagiza taasisi za umma kutekeleza maagizo anayoyatoa kwenye Mikutano ndani ya siku 14*


*Aagiza Halmashauri kushirikiana na Wizara ya Ardhi kumaliza Mgogoro wa ardhi kwenye kijiji cha Nyambitilwa*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe CPA Amos Makalla amewataka Watendaji wa Kata kutenga siku maalum ndani ya juma mayhalani Alhamisi kwa ajili ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi na kuwasilisha muhtasari wa zoezi hilo kwa Mkurugenzi wa Mtendaji mara moja.

Ametoa agizo hilo leo Oktoba 19, 2023 wilayani Magu akiwa kwenye Mkutano wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi ambapo amebaini msingi wa migogoro na kero nyingi unatokana na kulimbikizwa kwa dukuduku kwa wananchi kukosa msaada wanapohitaji kutoka kwa watendaji hao.


Aidha, CPA Makalla amesema amegundua kuwa uwajibikaji wa watendaji wa vijiji na kata umekua wa kusuasua na ndio maana hata kwenye mikutano yake ya kusikiliza kero mahudhurio ya wataalam hao yamekua hafifu hususani Magu ambapo alipokua akianza usikilizaji wa kero kulikua na watendaji 10 tu Kati ya 25 waliopaswa kuwepo.


"Nataka watendaji muwajibike sikubaliani na hali ya kuchukulia mzaha kwenye mambo ya msingi, hapa mlipaswa muwepo watendaji 25 lakini ni kumi tu ndio wamefika hapa maana yake hawataki kufahamu matatizo ya wananchi wao na ndio tunaona migogoro inazidi kuongezeka kila siku wataki walipaswa kuimaliza huko." Mkuu wa Mkoa.

Vilevile, amewataka watendaji wa Halmashauri na Taasisi zingine kukamilisha utekelezaji wa Maagizo na maelekezo anayoyatoa kwenye mikutano ya kusikiliza kero ndani ya siku 14 ili kutoa majibu ya kila suala lililoibuliwa na kuhitaji ufuatiliaji au utekelezaji kwa kutumia nyaraka au vielelezo mbalimbali.

"Watendaji naendelea kuwataka mtoke maofisini mkasikilize na kuhudumia wananchi, mtumie lugha ya staha yenye kujenga matumaini ili kujenga imani na uaminifu kwa wananchi ambao Rais Samia amejipambanua kuwa yupo kwa ajili ya kuwaboreshea huduma." Amesema.

Katika kutatua kero iliyowasilishwa na Ndg. Renatus Madoshi ya wananchi kutakiwa kulipa kodi ya ardhi kwenye kijiji cha Nyambitilwa ambapo mwaka 2009 halmashauri ililitwaa eneo lao (Mashamba) na kurasimisha na baadae kushindwa kulipa fidia na 2020 kuamua kulirudisha kwa wananchi ,Mhe. Makalla ameiagiza halmashauri kuwasilisha kero hiyo kwa Waziri wa Ardhi kwa ajili ya utatuzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.