• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA AZINDUA RASMI USIKILIZAJI WA KERO ZA WANANCHI MWANZA

Posted on: September 18th, 2023

RC MAKALLA AZINDUA RASMI USIKILIZAJI WA KERO ZA WANANCHI MWANZA


*Aagiza kwa wakuu wa Wilaya kila siku ya alhamisi iwe ya kusikiliza kero za wananchi


*Atoa agizo kwa Maafisa kutoa ushauri wa kisheria mapema kwa wananchi kabla ya shauri kufikishwa Mahakamani*


*Awataka watumishi kuwa na uwajibikaji wenye tija wa kusikiliza na kutoa maamuzi  kero za wananchi


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla leo Septemba 18, 2023 amezindua rasmi zoezi la kusikiliza kero za wananchi Mkoani humo na ametoa maagizo kwa wakuu wa Wilaya kila siku ya alhamisi iwe ya kusikiliza kero za wananchi kwa kuwasikiliza na kutoa maamuzi

Akizindua kampeni hiyo kwenye viwanja vya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa akiambatama na Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na viongozi wa taasisi mbalimbali za Serikali CPA Makalla amebainisha utaratibu huo ulkifanyika kikamilifu utaondoa kero nyingi za wananchi na kutowafikia viongozi wa juu wanapokuja kuwatembelea maeneo yao.

"Nimeunda kikosi kazi cha kuzungukia Wilaya zote kupokea taarifa za migogoro ya ardhi lakini niwahimize maafisa ardhi  toeni mapema ushauri wa kisheria kwa wananchi hali itakayowasaidia kupata haki zao mapema," amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Ameongeza kuwa kumekuwa na kero kubwa kwa wananchi hasa eneo la ardhi ambapo idadi kubwa wamekuwa wakipoteza haki zao kutoka kwa baadhi ya watu wenye uwezo ambao wamekuwa wakikimbilia mahakamani na kushinda mashauri husika kutokana na wananchi kushindwa kupata tafsiri vizuri za kisheria na kujikuta wakipoteza haki zao.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa ufafanuzi usikilizaji wa kero hizo siyo kwa mashauri ambayo tayari yametinga mahakamani kwani kisheria hana mamlaka ya kuingilia mhimili huo,hivyo amewataka wananchi kuwasilisha matatizo yao ambayo hayajafika kwenye vyombo vya sheria.

"Leo nafanya uzinduzi huu nikiamini mmepata somo la kujifunza namna ya kushughulikia kero za wananchi, sitarajii nikifika kwenye Halmashauri zenu nikute idadi kubwa ya wananchi wenye kero na badala yake mkafanye kazi hii kwa umakini na utatuzi haraka",amesisitiza CPA Makalla kwa viongozi.

Katika uzinduzi huo wa kusikiliza kero za wananchi kutoka Wilaya za Nyamagana na Ilemela,wananchi wengi waliojitokeza walikuwa na kero za ardhi ambazo baadhi mashauri tayari yalikuwa mahakamani na kero zingine Mkuu huyo alizipatia ufumbuzi hapo hapo.

Baada ya uzinduzi huo Wakuu wa Wilaya wote kutoka Mkoani Mwanza wataendelea na zoezi hilo kwenye vituo vyao kwa kujipangia utaratibu wa siku za kusikiliza kero zao na kuzipatia ufumbuzi kuanzia kwenye ngazi za vitongoji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.