• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA HAJARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI MRADI WA MAJI KISIWANI KOME, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

Posted on: January 16th, 2024

RC MAKALLA HAJARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI MRADI WA MAJI KISIWANI KOME, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA


*Amtaka Mkandarasi kuweka mkakati wa ukamilishaji mara moja*


*Asema ni uzembe kutokamilisha mradi huo tangu Agosti, 2023*


*Ataka nguvu zaidi kuwekwa kwenye ujenzi wa chanzo cha mradi huo*


*Aagiza kuwekwa mpango wa chakula shuleni ili kuwa na mahudhurio bora*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amemtaka Mkandarasi Kamba's Group of Companies Ltd anayejenga mradi wa maji wa Bugoro- Lugata kwenye Kisiwa cha Kome kukamilisha mradi huo ifikapo Mwishoni mwa mwezi februari mwaka huu.

CPA Makalla ametoa agizo hilo mapema leo Januari 16, 2024 akiwa ziarani kisiwani humo baada ya kukagua mradi huo unaotekelezwa kwa zaidi ya Bilioni 2.2 na kubaini uzembe kwenye utekelezaji uliopelekea kutokamilika kwa mujibu wa mkataba tokea mwezi Agosti 2024 huku msimamizi na Mkandarasi wakigubikwa na visingizio.


"Nataka niwaambie nyie (RUWASA), mkiendelea kucheka na wakandarasi wa namna hii mtatukwamisha, nataka ndani ya wiki moja Meneja RUWASA wa Wilaya unipe taarifa ya mpango wa kukamilisha mradi huu ifikapo mwezi ujao mwishoni, nataka Meneja na Mkandarasi mtimize wajibu wenu kuanzia sasa." Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Mkoa amesema kupitia mpango wa maendeleo ya maji (WSP) chini ya Programu ya usambazaji Maji vijijini na Usafi wa Mazingira (RWSSP) Mhe. Rais ameamua kuwaondolea adha wananchi zaidi ya elfu 30 wa kisiwani humo hivyo ni lazima mkandarasi huyo kwa kushirikiana na msimamizi watimize wajibu kwa kukamilisha mradi.

Awali, Mhandisi George Genes wa RUWASA alibainisha kuwa mradi huo umefikia asilimia 75 ya ujenzi na kwamba unahusisha ujenzi wa matanki 2, chanzo, ulazaji bomba, vituo 20 vya kuchotea maji na Uunganishaji maji kwa wananchi 200 walio ndani ya mita 30 na kwamba utanufaisha vijiji 7 vya kisiwani humo.

"Wewe ni mchapakazi kweli kweli yaani una muda mfupi Mwanza ila umeweza kufika kwenye kisiwa hiki wakati wengine hawakufika hapa kabisa, tunashukuru sana kwa mradi huu kwani wananchi wa Kome wameishi kwenye shida ya naji kwa miaka mingi." Mhe. Musa Abdalah, Diwani kata ya Bugoro.

Katika wakati mwingine Makalla ameridhishwa na uandikishaji wa wanafunzi wa awali na darasa la kwanza kwenye shule ya Msingi Muungano na ameagiza halmashauri kuweka mpango wa kuwa na chakula shuleni ili kutoa hamasa kwa watoto kuhudhuria masomo na kukamilisha ujenzi wa madarasa kutokana na uwepo wa maboma shuleni hapo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.