• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA: VIWANJA NA. 194 NA 195 KITALU U, RWAGOSORE NI MALI YA SERIKALI

Posted on: August 10th, 2023

RC MAKALLA: VIWANJA NA. 194 NA 195 KITALU U, RWAGOSORE NI MALI YA SERIKALI


*Asimamisha ujenzi uliokuwa ukiendelea baada ya  kampuni inayojenga kukaidi agizo la Mkurugenzi wa jiji*


*Asema umilikishaji wa viwanja uligubikwa na Ukiukwaji wa Sheria za nchi*


*Athibitisha uchunguzi umekamilika na wote waliohusika  na uazaji na umilikishaji viwanja hivyo watafikishwa katika vyombo vya sheria*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. CPA  Amos Makalla amemtaka anayejenga kwenye viwanja namba 194 na 195 Kitalu U Mtaa wa Rwagosore Jijini Mwanza kusimamisha Ujenzi na kuondoka mara moja kwani Viwanja hivyo ni Mali halali ya Serikali na si vinginevyo.

CPA Makalla ametoa agizo hilo mapema leo Agosti 10, 2023 alipofika kwenye eneo hilo katika kufuatilia Utekelezaji wa Agizo la Serikali la Julai 20, 2023 lililomtaka anayejenga kusitisha kazi zote kufuatia umilikishaji wake kugubikwa na ukiukwaji wa sheria ya ardhi na taratibu za nchi.

"Tarehe 20 mwezi wa Saba mlipewa taarifa ya kusitisha ujenzi lakini mmekaidi na mmekua mkiendelea na ujenzi usiku na mchana sasa nimekuja kuwaambia kwa mara ya mwisho kwamba Muondoka na kuanzia leo jengo hili litakua chini ya Usimamizi wa jeshi la polisi." Mhe. Mkuu wa Mkoa.

Amesema Uuzwaji wa Viwanja hivyo uligubikwa na Mizengwe iliyopelekea mgogoro ambapo Serikali iliunda Kamati iliyopendekeza kufanyika kwa taratibu za Urejeshwaji wa Hati iliyomilikishwa baada ya kughushi nyaraka za Serikali na ujenzi ulisimame.

"Hili jambo la viwanja namba 194 na 195 kwenye Kitalu U Mtaa wa Rwegosore linajulikana na kamati iliundwa na ikatolea Mapendekezo ambayo serikali inaendelea kuyatekeleza katika kuhakikisha mgogoro huu unafika mwisho." Mhe. Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amebainisha kuwa wote waliohusika kughushi nyaraka kwenye umilikishwaji wanachukuliwa hatua kutokana na utovu wa nidhamu na kwamba tayari Kamati ya Mipango Miji ilishavunjwa na unafanywa mchakato wa kuunda kamati ingine.

"La kwanza Viwanja hivi 194 na 195 (Kitalu 7 Rwegosore) ni mali halali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mchakato wa umilikishaji kwa anayejenga ulikiukwa na ulikua batili na ndio maana tunaendelea na mchakato wa kurejesha Hati" Amesisitiza Mhe. Makalla.


Vilevile, amefafanua kuwa TAKUKURU waliagizwa kuchunguza sakata hilo ili wote waliohusika kwenye suala hilo ovu wachukuliwe hatua na taratibu zinaendelea ambapo wakati wowote waliohusika watafikishwa Mahakamani.


"Umilikishwaji wa Mmiliki huyu haukua halali ulikumbwa na Miizengwe na mimi kama Mkuu wa Mkoa nipo kusimamia amani kwenye eneo langu na nitahakikisha ninalinda Mali za Serikali.

"Kuanzia sasa eneo hili litalindwa saa 24 na jeshi la Polisi na tusione mtu yeyote anaendelea na kazi baada ya tamko langu hivyo nataraji hakutakua na mtu yeyote anafanya kazi kwenye eneo hili." Amesisitiza Makalla

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.