• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ahimiza ushirikiano wa kimaendeleo na viongozi wa Kimila Mwanza

Posted on: May 11th, 2023

*RC Malima ahimiza ushirikiano wa kimaendeleo na viongozi wa Kimila Mwanza


Viongozi wa Kimila wa Mkoani Mwanza wameombwa kuushirikisha uongozi wa Mkoa  katika kazi zao pamoja na mambo ambayo yakipata ushirikiano wa Uongozi yanaweza kuleta maendeleo katika Mkoa huo.

Wito huo umetolewa leo Mei 11, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima wakati alipokutana na Viongozi wa Kimila wa Mkoani humo katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

" Kama yapo mambo ambayo yanahusiana na mafanikio katika kazi zenu basi naomba mnishirikishe  hata katika mambo yote ambayo yanaweza kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa watu wa Mwanza na kanda ya Ziwa kwa ujumla," RC Malima

Aidha Mhe. Malima ameongeza kuwa  serikali ya Mkoa kwa kushirikiana na Chuo cha Mt. Augustino (SAUT) wanampango wa kuanzisha (Kituo cha Ubunifu cha Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia) ili kiweze kuwasadia  wananchi wa Mkoa huo.

 Serikali ya  Mkoa  imeamua kufanya kampeni mahususi  ili kujaribu kuwafikia wananchi wake kwahiyo kuna kituo cha kuhamasisha maendeleo ya kiuchumi( Kituo cha Ubunifu cha Maendeleo na Sayansi na Teknolojia) ambacho tunataka tukianzishe kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Mt. Augustino (SAUT)," Amesema Mkuu huyo wa Mkoa

Naye Mtemi. Charles Itale wa kwanza wa  Bujashi Magu na  Mwenyekiti wa Umoja wa Watemi Mkoa wa Mwanza  ameongeza kiwa kitu kinachosababisha mmomonyoko wa maadili ni kuchukulia swala la malezi kama jukumu la mtu mmoja na sio la jamii kwa ujumla jambo ambalo linaleta utofauti na zamani

Pia  Mtemi. Domina Musiba wa Tatu wa Buchosa amewaomba viongozi wa kiserikali na wa kidini waweze kusimamia maswala ya kimaadili na pia wapate wasaa wa kuielimisha jamii pale wanapokutana nayo ili waweze kurudisha maadili kama kipindi cha zamani

"Tunaomba sana viongozi wote wa dini hata wa Serikali  wanapokutana na wananchi waweze kusimama na kutoa elimu kuhusu mambo ya maadili kwa jamii na  pia wajenge uhusiano mzuri na Watemi ili tuweze kukutane na  kuuzungumza kuhusu maadili na mienendo ya jamii zetu kwa ujumla.

Mkutano huo wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na viongozi wa kimila ulilenga kujadili maswala ya mmomonyoko wa maadili katika jamii na kujadili juu ya tamasha la bulabo ambalo ni maalum kwa ajili ya  kusherehekea mavuno kwa mila za kabila la Kisukuma ambazo zitafanyika Juni 11 hadi 17 2023 katika kata ya  kisesa wilaya ya Magu.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.