• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aivunja Kamati ya usimamizi ya Jengo la abiria uwanja wa Ndege Mwanza

Posted on: August 7th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima ameivunja Kamati ya usimamizi ya ujenzi wa Jengo la abiria la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwanza kutokana na ubadhirifu wa fedha za Mradi huo.

Akizungumza  leo na wahusika wa Mradi huo wa Jengo la abiria mara baada ya kulifanyia ukaguzi Mkuu huyo wa Mkoa amesema baada ya kuivunja kitakachofuata ni kupata taarifa za kina za kila muhusika ili kujirudhisha uwezo wao.

"Hainiingii akilini kuona taarifa inayosema Mkandarasi Mshauri Berno Balinamomi amepata kazi hiyo bila mkataba kwa zaidi ya Shilingi milioni mia moja na kufanyika malipo yaliyopitiliza gharama halisi" amesema Mkuu huyo wa Mkoa.

Amesema huyo Mkandarasi Mshauri licha ya kulipwa pesa nyingi amefanya makosa mengi katika ujenzi huo kiasi cha kupoteza sifa ya Jengo hilo kuwa na hadhi ya Kimataifa.

Amesema baada ya kuivunja Kamati hiyo atashirikiana na Katibu Tawala wa Mkoa Balanda Elikana kuunda Kamati mpya itakayowashirikisha Wataalamu wa ujenzi na  viongozi wa vyombo vya Ulinzi na usalama.

Mhe Malima amemtaka Mkandarasi huyo kurekebisha kasoro zote na Jengo hilo kumalizika haraka ili Mkoa wa Mwanza ambao upo Kimkakati upokee Watalii wanaozidi kuvutiwa na Vivutio vingi vya Kitalii vilivyopo Mkoani humo na Mbuga ya Serengeti.

Jengo la abiria lenye gharama ya zaidi ya Shilingi Bilioni 13 linalojengwa kwa kuchangiwa gharama na Halmashauri mbili za Nyamagana iliyotoa zaidi ya Shilingi Bilioni 2 na Ilemela iliyotoa zaidi ya Shilingi Bilioni 1 na nyingine kuongezwa na Serikali Kuu hadi sasa zimeshatumika Shilingi Bilioni 8.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.