• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima akabidhiwa Vikombe vya Ubingwa UMISETA na UMITASHUMTA kwa Mkoa wa Mwanza

Posted on: August 30th, 2022


Mhe. Adam Malima, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewapongeza wanafunzi wa shule za msingi na Sekondari kwa uwakilishi mzuri kwenye Mashindano ya  Michezo ya Shule za Msingi na Sekondari ambapo Mkoa huo umeibuka Mshindi wa kwanza Kitaifa kwa Michezo ya UMITASHUMTA na wa Pili kwa UMISETA.

Mhe. Malima amesema hayo leo Agosti 29, 2022 wakati wa hafla ya kukabidhi vikombe 16 vya ushindi kwa michezo mbalimbali ya wanafunzi kwa Shule za Msingi (UMITASHUMTA) na Sekondari (UMISETA)  kufuatia michezo iliyofanyika Kitaifa Mkoani Tabora mapema mwezi Agosti 2022.

"Napenda niwapongeze sana kamati nzima kuanzia walimu waliofanya maandalizi, wadau wetu, mameneja na waratibu wote lakini pongezi zangu za dhati kabisa ni kwa wanamichezo wenyewe waliotuletea vikombe hivi leo." Malima.

Aidha, ametoa wito kwa wazazi kuendeleza vipaji vya watoto wao na kuwaendeleza kila wanapoonesha uwezo kwenye michezo kadhaa ili kukuza vipaji na kuwafanya wanafunzi kuwa wachezaji wazuri wanapomaliza shule na kuweza kujiimarisha hata kiuchumi kupitia michezo mbalimbali.

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Balandya Elikana amewapongeza walimu na wanafunzi wote walioshiriki maandalizi na Mashindano ya shule za Msingi na Sekondari mkoani humo na ametoa rai kwao kuendelea mbele katika nyanja za kitaaluma kupitia chachu ya Michezo hiyo.

"Ninafurahi kuwa juhudi zenu zimetufikisha hapa na ni matumaini yangu kuwa ushindi kwenye michezo tutautafsiri kwenye matokeo mazuri kitaaluma katika kila shule mkoani hapa" Amesema, Mwalimu Elias Nkwabi, Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza.

Afisa Michezo Mkoa wa Mwanza, William James amesema wanafunzi 240 wameshiriki michezo hiyo Kitaifa Mkoani Tabora na kushika nafasi ya Kwanza kwa michezo ya UMITASHUMTA na nafasi ya pili kwa UMISETA ikiwa ni matunda ya maandalizi mazuri yaliyofanywa na kamati na Mashindano.

Kupitia hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa amekabidhiwa vikombe vya ushindi kupitia michezo ya Ngoma, Mpira wa Miguu, Mpira wa Pete, Kikapu wavulana, Kwaya, Riadha Wavu wavulana, wavu wasichana, Soka wasichan, Riadha wasichana, Mpira wa Mikono wavulana na Kikombe cha ushindi wa jumla kwa UMITASHUMTA.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.