• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima akipongeza Chama cha Madaktari wa tiba za Wanyama kwa kutoa elimu hiyo kwa wanafunzi wa kike Mwanza

Posted on: April 29th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amekipongeza Chama cha Madaktari wa Tiba za Wanyama nchini TVA kwa kuyatumia Maadhimisho ya Kitaifa Mwanza ya siku ya utoaji huduma za afya ya wanyama, kwa kutoa elimu shuleni kuwahamasisha wanafunzi wa kike kuchangamkia taaluma hiyo.

Akizungumza kwa niaba yake leo wakati wa ufungaji wa Maadhimisho hayo kwenye viwanja vya Furahisha,Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala amesema kumekuwa na kasumba ya mfumo dume kuwa kazi hiyo ni ya wanaume kutokana na kuwakabili wanyama wengine wenye ukali na nguvu,jambo ambalo halina ukweli wowote.

"Tumemshuhudia Rais wetu Mhe.Dkt.Samia Suluhu akiweka mazingira mazuri ya kuwepo na shule maalum za wasichana  kuchukua masomo ya Sayansi,hii maana yake ni kutaka kuwepo na uwiano mzuri wa wataalamu wa kike wa kulijenga Taifa letu".Amesema Mkuu huyo wa Wilaya.

Amewakumbusha pia wakazi wa Mwanza wenye mifugo kuyachangamkia Maadhimisho hayo kwa kupata elimu ya kutosha na kuona umuhimu wa chanjo za mara kwa mara za mifugo yao ili iwe  salama kwa mlaji na uhakika wa soko.

"Ndugu mgeni rasmi mbali ya kuhamasisha elimu hiyo shuleni,April 27 tumetoa huduma mbalimbali za mifugo bila malipo zikiwemo chanjo na upasuaji na kufikisha idadi ya mifugo 607 tuliyohudumia siku hiyo maeneo ya Kisesa wilayani Magu,lengo likiwa ni kuwaelimisha wananchi kuwa na mifugo bora wakati wote,"James Kawamala,Katibu wa TVA Taifa.


"Maadhimisho haya Kitaifa tumeyafanya kwa mara ya kwanza na tukachagua Mkoa Mwanza ambao una sifa ya kuwa na wafugaji wengi,hivyo tumefarijika elimu tuliyotoa itakuwa na tija kwao na Taifa kwa ujumla," Prof.Esron Karimuribo,mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Kila ifikapo wiki ya mwisho ya April,Tanzania hujumuika na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya utoaji huduma za afya ya wanyama ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni Kukuza utofauti,usawa na ushirikishwaji katika taaluma ya tiba ya wanyama.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.