• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aridhishwa na ujenzi wa Miradi ya Kimkakati Mwanza

Posted on: September 2nd, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amemtaka Mkandarasi anayejenga Mradi wa Soko Kuu la Kisasa Mohamed Builders Company Limited na Halmashauri ya Jiji la Mwanza kuweka mipango thabiti ya kukamilisha Mradi huo ili kuepusha gharama zisizotarajiwa endapo utatakelezwa kwa muda mrefu zaidi na uweze kuwahudumia wananchi kwa haraka.

Mhe. Malima ametoa agizo hilo sokoni hapo  Septemba Mosi 2022 alipoungana na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza Mhe. Anthony Dialo kwenye ziara ya kukagua Ujenzi wa Miradi ya Kimkakati.

"Mimi binafsi nimeridhishwa sana na mpango wa mradi huu maana una nia ya kupandisha maisha ya wananchi kuwa ya kisasa na tumeona kuwa umegharimu zaidi ya Tshs Bilioni 20, hizi fedha nyingi sana hivyo basi huduma zitakazotolewa hapa ni lazima zilenge kuwasaidia wananchi hasa wafanyabiashara wadogo." Amesema Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Mkuu wa Idara ya Kilimo na Ushirika Erick Mvati akimuwakilisha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji amefafanua kuwa zaidi ya  Tshs Bilioni 20 zitatumika kujenga mradi huo ulioanza kutekelezazwa  0ktoba 2020 na utakamilika ifikapo Septemba 30 2022 na kwa sasa umefikia asilimia 79 ya utekelezaji.

Aidha, amefafanua kuwa Mradi huo ulioajiri zaidi ya vijana 100 wakati wa utekelezaji, utasaidia kuongeza mapato kwenye Halmashauri hiyo na kupunguza utegemezi kutoka Serikali kuu kutokana na huduma kadhaa zitakazokuwemo zikiwemo mabenki, vizimba vya wafanyabiashara wadogo, eneo la wafanyabiashara wakubwa, michezo ya watoto na eneo la kuegesha magari zaidi ya 150.

Baada ya ukaguzi huo viongozi hao wamefika kwenye Bandari ya Mwanza Kusini na kukagua Ujenzi wa Meli kubwa ya kisasa ya MV Mwanza yenye uwezo wa kubeba Magari madogo 20, makubwa 3, tani 400 za mizigo na Abiria 1200 kwa wakati mmoja ambayo inatekelezwa na Mkandarasi Gas Entec kutoka Korea Kusini kwa Bilioni 70 wamepongeza utekelezaji wa Mradi huo na wamesisitiza ukamilishaji wa ujenzi huo kwa manufaa ya wananchi waishio kwenye ukanda wa maziwa makuu.

"Ujenzi wa hii Meli ulianza January 2019 na ulikua uende kwa miaka miwili lakini zilitokea changamoto nyingi ambapo mkataba uliongezwa hadi  Mei 2023 ambapo kwa sasa umefikia asilimia 71 ya ujenzi na hakuna meli kubwa kama hii kwenye ukanda wa maziwa makuu." Amefafanua Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Huduma za Meli, Erick Hamisi

Bwana Hamisi ameongeza kuwa Meli hiyo inajengwa kwa Tshs Bilioni 97 ambapo Chelezo yake imegharimu Bilioni 36 na mradi huu umeajiri watanzania 150 hadi 200 na wataalamu 6 tu kutoka nje na ifikapo Oktoba mwaka huu meli hii itaingizwa kwenye maji ambapo matengenezo mengine yataendelea ikiwa kwenye maji.

"Nimefarijika sana leo, awali wakati Mradi huu unaanza tulipokua na Michoro tu kwenye makaratasi ulikua ukisikia zile takwimu unadhani ni utani Rais Samia anatengeneza Miundombinu kwa ajili ya wananchi wake na hiyo ndio dira yake ya kuwatumikia wananchi na kwakweli ameamua kuhakikisha mambo hayasimami hivyo basi wananchi wa Mwanza wakae Mkao wa kusafiri nayo." Malima.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.