• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ataka adhabu kali na marekebisho ya Sheria za barabarani dhidi ya wanaosababisha ajali kwa uzembe

Posted on: March 17th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima ametoa wito kwa Wadau wa Usalama barabarani kuangalia namna ya kufanya mabadiliko kwenye baadhi ya Sheria za Usalama barabarani ili ziweze kutoa adhabu kali zaidi kwa wote watakaosababisha ajali kwa uzembe.

Mhe. Malima amebainisha hayo mapema leo Machi 17, 2023 wakati wa hafla ya Kufunga Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani Kitaifa yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Furahisha jijini Mwanza kuanzia tarehe 14 Machi, 2023 ambapo yalifunguliwa na Mhe. Waziri Mkuu wa Tanzania.

"Ajali nyingi za Barabarani zinatokea kutokana na uzembe wa kujitakia kama kuendesha vyombo vya moto kwa muda mrefu bila kupumzika, kuendesha chombo wakati umelewa na mwisho kusababisha vifo vya raia na kupoteza nguvu kazi ya Taifa" Mhe. Malima.

Vilevile, ametoa rai kwa waendesha Pikipiki za abiria (Bodaboda) kuzingatia sheria za Usalama wawapo kwenye shughuli zao kwani eneo hilo limekua chanzo kikubwa zaidi cha ajali na kwa askari wa barabarani amewataka kuwajibika ipasavyo ili kulinda maisha ya wananchi.


Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Usalama barabarani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi amebainisha kuwa pamoja na Jeshi la polisi kutembelea Shule za Msingi na Sekondari, makundi mbalimbali ya watumia vyombo vya moto Mkoani humo wamepewa Elimu ya Usalama barabarani.

Naye, Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Mabaraza ya Usalama barabarani ambaye pia ni mwenyekiti wa Mkoa wa Kipolisi Kinondoni Idd Azzan ametumia wasaa huo kulihakikishia Jeshi la Polisi na wananchi kuendelea kutoa elimu ya Usalama barabarani kila wakati ili kuhakikisha jamii inakumbushwa wakati wote juu ya umuhimu wa kuzingatia sheria za Usalama kila watumiapo barabara.

"Nia yetu kubwa ni kuhakikisha ajali kama hazitaondoka kabisa basi zinapungua hivyo nawasihi watumiaji wa Miundombinu ya barabara kufuata sheria za usalama ili kuhakikisha wanakua salama barabarani na waweze kuwalinda watumiaji wengine wa barabara." Amesema mwenyekiti.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.