• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima ataka mashindano ya Mitumbwi yawe na sura ya kimataifa

Posted on: December 12th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka waratibu wa Mashindano ya Mitumbwi kuongeza ubunifu ktk mchezo huo ili kuwapatia washiriki bora watakaomudu ushindani wa kimataifa.

Akizungumza mwishoni mwa wiki iliyopita Mwaloni Kirumba kwa niaba yake, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala amesema michezo ukiwemo huo wa Mitumbwi imekuwa nguzo imara ya ajira na kuwafanya wanamichezo kuwa na kipato kikubwa hivyo kuna kila sababu ya kuwajengea mazingira  ya kisasa wanamichezo hao kuwa wa kimataifa.

"Nawapa Rai waandaaji wa Mashindano haya ambayo yanafanyika kila mwaka hapa Mwanza,hawa wanazofanya vizuri wasiishie kuwapa zawadi ya pesa tu na kuja kuwatafuta mashindano yajayo hii ni sawa na kutoutendea haki mchezo huu na wachezaji husika Mhe.Masala.

Amesema mashindano haya sasa huu ni mwaka wa 14 tangu yaanzishwe,waandaaji sasa muone kuna kila sababu ya kuyatoa nje ya mipaka yetu ambapo huko hawa wachezaji watazidi kupata fursa ya ushindani wa juu na kupata timu za kulipwa ambayo ndiyo yawe malengo yetu na siyo kuishia hapa hapa tu.

Aidha amewapongeza waandaaji hao kwa kuzidi kuupa hamasa mchezo huo kiasi cha kuwa na mvuto kwa wakazi wa Mwanza na kutoa nafasi ya kuutangaza Mkoa huo Vivutio vingi vyenye fursa mbalimbali ikiwemo rasilimali ya maji ya Ziwa Victoria.

Naye msimamizi wa bodi ya Utalii Kanda ya Ziwa Gloria Muhambo amewahakikishia washiriki wa mchezo huo kuzidi kupewa ushirikiano kutokana na mashindano hayo kutoa ujumbe wa Vivutio vya Kitalii vilivyopo ndani ya Mkoa wa Mwanza.

"Tumeshuhudia uwezo mzuri wa kupiga makasia kwa washiriki wanaume na wanawake,naamini tutakapo wapa fursa ya ushiriki wa kimataifa Mkoa wetu utazidi kung'ara.

"Mkakati wetu sasa na kuyashirikisha Mataifa ya ukanda wa Maziwa Makuu kuwashindanisha wanamichezo wetu lengo likiwa ni kuwafungulia fursa za kuchomoza Kimataifa" Ludovick Kanyebuye mratibu wa mashindano ya mitumbwi Mkoa wa Mwanza.

Naye mratibu wa mashindano hayo kutoka Kampuni ya SCOPE inayosimamia mashindano hayo Benard Mweta amebainisha wamejipanga kuhakikisha mashindano yanakuwa bora na kuzidi kuviinua na kuvikuza vipaji vya washiriki ili waje kuwa washindani wa kimataifa

Katika mashindano hayo timu za kutoka Misungwi zimetoka kimaso maso kwa wanaume na wanawake kutokana na kushika nafasi za kwanza hadi tano,ambapo mahindi wa wanza amekunja kitita cha Shs milioni mbili,wa pili milioni moja na nusu,wa tatu milioni moja huku mshindi wa nne akitoka na laki 8 na wa tano akipata laki 5

Mashindano hayo yameshirikisha jumla ya timu 78,Wanawake wakiwa 18 kutoka Mara,Ukerewe,Misungwi na wenyeji Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.