• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mongella agawa vitambuliaho vya wajasiriamali wadogo kwa Halmashauri

Posted on: June 15th, 2020

Mkoa wa Mwanza umetoa vitambulisho vya wafanyabiashara wadogo  (Machinga) na watoa huduma wadogo elfu 73,000 kwa awamu ya pili mwaka huu,kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri na  Wilaya zote .
Ambapo awamu ya kwanza walikabidhiwa vitambulisho 15,000 vya wafanyabiashara wadogo (Machinga ) vyenye thamani ya million 300 ambapo vilivyogawiwa ni 7,792 sawa na asilimia 51.95 huku vitambulisho 7,208 sawa na asilimia 48.05 vikiendelea kugawiwa na  kiasi cha fedha cha milioni 155.84 (Tsh.155,840,000) zikiwasilishwa TRA.
Akizungumza wakati akiwakabidhi vitambulisho hivyokutoka ofisi ya Rais Tamisemi vilivyopitia Mamlaka ya Mapato Tanzania “TRA” Mkuu wa mkoa wa Mwanza John Mongella aliwataka viongozi hao  kuhakikisha fedha zote zinakwenda benki

Anasema  jumla ya vitambulisho vilivyopokewa Mkoa wa Mwanza  ni 88,000 vyenye thamani  ya billion 1.76, hivyo hadi sasa kwa awamu ya kwanza wameuza kwa asilimia 54 na amewataka kuhakikisha zoezi hilo wanalifunga ndani ya wiki moja pia waratibu wawe makini kwa sababu mfumo umeboreshwa na  unafanyakazi ipasavyo hivyo kula hela ya serikali haiwezekani.

" Vitambulisho ni Jambo vyeti sana hivyo tulitilie mkazo vinaweza kukupotezea mwelekeo kwa ushauri wangu vitambulisho hivi tulivyowagawia awamu ya pili tuvimalize mwezi wa nane "anasema Mongella.
Anasema vitambulisho visikae Halmashauri bali vifike kila sehemu kwa sababu Mhe.Dkt. Rais Magufuli alitoa ahadi kwa wananchi kuhusiana na vitambulisho hivyo, ni wakati wa kufanya  kazi ili kuleta matokeo yanayoonekana.

" Ninawapongeza Magu, Kwimba na Misungwi kwa kuanzia wamefanya kazi nzuri na wameonyesha njia kufikia leo jioni naimani Magu  mtakuwa mmepiga asilimia 100 kwa awamu ya kwanza" anasema Mongella.
Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Emmanuel Tutuba,alisema vitambulisho hivyo vya awamu ya pili  wamevipokea kutoka kwa Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mwanza vimegawiwa katika halmashauri 8 na Wilaya 7 za mkoa huo ikiwemo  halmashauri ya Jiji la Mwanza wamepokea vitambulisho 20000,Ilemela 18000,Sengerema 6000,Buchosa 6000,Ukerewe 5000,Kwimba 6000,Misungwi 6000 na Magu 6000 .
Naye Kaimu Meneja wa TRA mkoa wa Mwanza Hoseya Kidasi anasema  hii ni awamu nyingine ya kutoa vitambulisho ambapo tumekabidhi jumla ya vitambulisho 73,000 hivyo tunaunga mkono hatua zinazochukuliwa na Mkoa pia tutatatua changamoto ya mtandao ili kutoleta vikwazo na tutaongeza juhudi na kushirikiana ipasavyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza Kiomoni Kibamba,anasema changamoto waliyokutana nayo ni wakati wakifanya ukaguzi wa vitambulisho kwa wafanyabiashara hao unakuta wamachinga wa eneo moja ambao wanavitambulisho wanaenda na eneo jingine,hivyo alitoa ushauri kuwa awamu nyingine vitambulisho viwekwe picha ya walengwa ili kuondoa changamoto hiyo.

"Biashara nyingi zipo mjini tunafanya matangazo ya gari ,na spika kwenye mitaa na tunatembea kuviuza kasi siyo nzuri tunachokiitaji ni kutumia nguvu kidogo " anasema Kibamba.




Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.