• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA KUONGEZWA KWA VIFAA NA NGUVUKAZI KUKAMILISHA UJENZI KITUO CHA MICHEZO MALYA

Posted on: January 13th, 2025

RC MTANDA AAGIZA KUONGEZWA KWA VIFAA NA NGUVUKAZI KUKAMILISHA UJENZI KITUO CHA MICHEZO MALYA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka kampuni ya CRJE (East Africa) Limited inayojenga mradi wa kituo cha michezo cha umahiri Malya Wilayani Kwimba kuongeza nguvukazi na vifaa ili kuharakisha ujenzi huo.

Mhe. Mtanda ametoa agizo hilo leo Januari 13, 2025 wakati alipofanya ziara chuoni hapo na kusema  Mkandarasi alipaswa kukamilisha mradi huo tarehe 16 mwezi huu kwa mujibu wa mkataba lakini ameshafanya kazi kwa asilimia 14.7 tu na kumpa onyo kwamba Serikali haitomvumilia endapo atachelewesha mradi huo.

Ameongeza kuwa, Serikali imetenga fedha zaidi ya Tshs. Bilioni 31 ili kuimarisha sekta hiyo nchini kwa kupata vifaa na miundombinu ya kisasa hivyo mkandarasi hatovumiliwa atapoonekana na lengo la kukwamisha juhudi hizo.

" Mkandarasi au mtu yeyote aliye hapa anaweza kujionea kwa macho ya kawaida tu kwamba vifaa na nguvukazi zilizopo hapa havioneshi dhamira ya kutaka kukamilisha mradi huu kwa haraka, sasa naagiza muongeze kabla sijawachukulia hatua."

Katika kufuatilia hilo kwa karibu, Mhe. Mtanda amemtaka mkandarasi kuketi pamoja na mshauri, uongozi wa Wilaya na chuo na kuwekeana ratiba ya kazi ambayo itafuatwa kila wakati na kuhakikisha wanaifuata na kuitekeleza.

Awali, msimamizi wa mradi huo mhandisi Feisal Msingwa alibainisha kuwa mkandarasi ameshalipwa malipo ya awali Tshs. Bilioni 3.1 na muda wa utekelezaji wa mradi huo ni mwaka mmoja (Miezi 12) kutoka Januari 2024 hadi Januari 2025 lakini alisimama kazi kwa muda wa miezi minne kutokana na ucheleweshaji wa malipo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.