• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAHIDI KUWA MLEZI BORA KWA MAAFISA USAFIRISHAJI WA SERIKALI

Posted on: March 2nd, 2025

RC MTANDA AAHIDI KUWA MLEZI BORA KWA MAAFISA USAFIRISHAJI WA SERIKALI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amefungua kongamano la Maafisa usafirishaji wa Serikali mkoani humo na kuwaahidi kuwa mlezi bora wa chama chao ili kiweze kufikia malengo waliyojiwekea.

Akizungumza nao leo Machi 2, 2025 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa Mtanda ambaye ni mlezi wa chama hicho amewakumbusha maafisa hao wa usafirishaji kuendelea na kutimiza wajibu wao wa kulinda usalama barabarani.


"Afisa usafirishaji tambua wewe ni mtu muhimu, tanguliza nidhamu kwa mkuu wako wa kazi, tunza siri na siku zote hakikisha chombo chako ni salama kabla ya kuanza kukitumia", Mkuu wa mkoa.

Vilevile, mlezi huyo amewataka baadhi ya viongozi wenye tabia ya kuwanyanyasa madereva kama vile kuwatumia muda mwingi pasipo sababu, kuingilia posho za mafuta waache tabia hiyo kwani haina tija zaidi ya kujenga chuki.


Aidha, katika mkutano huo Mkuu huyo wa Mkoa amekipongeza chama hicho kwa kuzidi kujiimarisha kwa kuwa na wanachama wengi kutoka idadi ya 80 hadi 183 na kawataka wale ambao bado hawajajiunga kutoka Ofisini kwake wafanye hivyo haraka.

"Nimesikia katika risala yenu baadhi ya changamoto zinazowakabili ikiwemo ukosefu wa Ofisi na kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi yenu,natoa maelekezo kwa Katibu Tawala kukaa na uongozi wenu ili kupatikane ufumbuzi na kikao kijacho nipate mrejesho",Mtanda.

Awali katika taarifa yake fupi kwa mgeni rasmi,Katibu wa chama hicho Mkoa,Juma Mago amebainisha bado wanachangamoto kwa baadhi ya waajiri kuwa wagumu kutoa ruhusa kuhudhuria mikutano yao pia amempongeza mlezi wao kwa kuwajali kwa vitendo hali iliyowafanya kuhudhuria kwa wingi katika mkutano wao wa Taifa uliofanyika mwaka jana Jijini Arusha.

Katika kongamano hilo RC Mtanda amekabidhiwa tuzo kutokana na mchango wake bora kwa maafisa usafirishaji wa Serikali mkoani Mwanza,na pia baadhi ya Taasisi za Serikali zimekabidhiwa vyeti kutokana na ushirikiano mzuri wanaotoa kwa chama hicho na wanachama wake

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.