• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AFAFANUA UKWELI WA KILICHOTOKEA SIKU YA MAZOEZI YA SIMBA-CCM KIRUMBA

Posted on: November 22nd, 2024

RC MTANDA AFAFANUA UKWELI WA KILICHOTOKEA SIKU YA MAZOEZI YA SIMBA-CCM KIRUMBA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda amekanusha taarifa ya uongo inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii inayotolewa na msemaji wa klabu ya Simba,Ahmed Ally kuwa ameingilia mazoezi ya Simba akiwa pamoja na askari wenye silaha na kuwataka wananchi na mashabiki kuipuuzia taarifa hiyo yenye nia ya kumchafua na kumvunjia heshima.

Mkuu huyo wa Mkoa amelazimika kuzungumza na vyombo vya habari mapema leo asubuhi Novemba 22,2024 Ofisini kwake baada ya kupokea ujumbe mwingi wa kuulizwa kuhusiana na uzushi huo,na kubainisha alichofanya yeye kwa nafasi yake kama Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa ni kwenda uwanjani baada ya kupokea taarifa ya kutaka kupigwa na makomandoo wa Simba na kujifungia vyumbani  wasimamizi wa Pamba Jiji kwenye uwanja huo ili wasiumizwe na kuanza  kuvunja vioo vya madirisha.

Mtanda amesema anatambua kanuni za soka na asingeweza kuingia uwanjani wakati ilikuwa ni siku ya mazoezi ya Simba na badala yake alikuwa nje ya uwanja akifanya mawasiliano na baadhi ya viongozi wa Simba ili wazungumze kuachiwa wasimamizi wa Pamba Jiji waliokimbilia vyumbani kuhofia kupigwa na makomandoo wa Simba.


"Jitihada zangu za kuzungumza na viongozi wa Simba ziligonga mwamba nikiwa nje ya uwanja hadi walipomaliza mazoezi yao na mlango kufunguliwa na askari kuingia na kuwafikisha kituo cha polisi aliyevunja vioo vya madirisha na wasimamizi wa Pamba Jiji kwa maelezo zaidi",amefafanua Mkuu wa Mkoa.

Ameongeza kuwa kutokana na sakata hilo Mwenyekiti wa klabu ya Simba Murtaza Mangungu baadaye alimpigia simu na kumuomba radhi kwa yote yaliyotokea na kuahidi kugharamia hasara iliyotokea ya uharibifu uwanjani hapo.


Mtanda amewaondoa hofu mashabiki wote na kuwataka kuendeleza mshikamano wa amani na kufurahia burudani ya kuzishuhudia timu kubwa za Simba na Yanga na kupuuzia uzushi huo ulioenezwa na msemaji wa klabu ya Simba Ahmed Ally ambao una nia ya kuwapa taharuki mashabiki kuelekea mchezo huo utakayopigwa leo Novemba 22,2024 kwenue uwanja wa CCM Kirumba.

Aidha Mtanda amebainisha yeye ataendelea kuwa mlezi na kushirikiana na  timu mbalimbali licha ya mahaba yake ya kuipenda Yanga kwani hivi karibuni aliwachangia fedha tawi la Simba walipokuwa wanajiandaa na tamasha  la Simba Day na amekuwa mlezi wa matawi yao sehemu mbalimbali alizofanya kazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.