• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AHIMIZA KULIOMBEA TAIFA, KUTENDA MEMA NA KUWAKUMBUKA WASIO NA UWEZO

Posted on: April 10th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA KULIOMBEA TAIFA, KUTENDA MEMA NA KUWAKUMBUKA WASIO NA UWEZO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Aprili 10, 2024 ameungana na waumini wa dini ya kiislamu katika swala ya Eid iliyofanyika kwenye uwanja wa Nyamagana na kuwakumbusha kuendelea kuliombea Taifa kujenga mshikamano, kutenda matendo mema na kuwakumbuka wale wasio na uwezo na hatimaye kupata thawabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Taifa la Tanzania limeendelea kuwa na amani kutokana na busara na hekima za viongozi wetu wa juu hivyo hakuna budi kuwaombea ili Mwenyezi Mungu awazidishie ari ya kuwatumikia vizuri Watanzania.

"Wapo baadhi ya watu wanapokuwa kwenye nafasi huzitumia vibaya iwe kwa dhuluma au uonevu wa aina yoyote mambo ambayo hayampendezi Mwenyezi Mungu aliyetuleta Duniani ili tumtumikie vyema na kurejea kwake tukiwa wasafi wa roho," Mkuu wa mkoa.

Mara baada ya kushiriki swala ya Eid Mhe. Mtanda akiongozana na Shekhe Mkuu wa mkoa wa Mwanza Hassan Kabeke pamoja na wadau benki ya NMB wakiwa kwenye Ofisi za Bakwata mkoa, wametoa zawadi ya sikukuu kwa vituo 11 vya watoto wanaoishi katika mazingira magumu kutoka wilaya Nyamagana na Ilemela zenye thamani ya shs milioni 2.6

"Mhe.mkuu wa mkoa tunakushukuru sana kwa tendo hili,hizi fedha ulizogharamia pengine ungeamua kula vizuri na familia yako,lakini ukaamua kuzitoa kwa ajili ya wengine,Mwenyezi Mungu azidi kukupa rehema zake," Shehe Kabeke.

Akimshukuru mkuu wa mkoa kwa zawadi hizo, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi amesema watoto hao wanaendelea kujiona ni wa famllia moja kutokana na Jamii kuwa nayo karibu kwa kuwapa misaada mbalimbali.

Akiwa katika Iftar iliyoandaliwa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe.Hassan Masala Jumanne hii jioni kwenye Hotel ya City Link,mkuu huyo wa mkoa amesema Ofisi yake ipo wazi wakati wote kuwasikiliza  wale wenye kero mbalimbali.

"Mimi siyo mkaaji wa ofisini bali nitawafuata huko mlipo wananchi na wale mtakaofika ofisini kwangu mjisikie huru kuniona lakini sitaki kuletewa taarifa chonganishi," amesisitiza Mhe.Mtanda wakati akitoa hotuba fupi mara baada ya Iftar.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.