• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AHIMIZA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI

Posted on: July 15th, 2024

RC MTANDA AHIMIZA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA ZA MAPATO YA NDANI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Halmashauri ya Jiji la Mwanza kutumia fedha za mapato ya ndani kwa mujibu wa sheria ikiwemo kuhakikisha zinapelekwa kwenye miradi ya maendeleo ili kusogeza huduma kwa wananchi.

Ametoa agizo hilo leo tarehe 15 Julai, 2024 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza wakati akizungumza na Viongozi wa Serikali, watumishi na wadau wa maendeleo wilayani Nyamagana.

Mtanda amesema, kwa mujibu wa makusanyo ya fedha kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2024 halmashauri  hiyo inapaswa kupeleka shilingi Bilioni 10 kwenye miradi ya maendeleo lakini wamepeleka Bilioni 8 hivyo ameagiza kupelekwa kwa bilioni 2 zilizobaki.

"Ukitaka kujua mimi ni nani, chezea fedha za miradi, yaani mradi usipokamilika wakati fedha zipo ni lazima nikupeleke TAKUKURU, sitakuacha maana hauwatakii mema wananchi ambao wanasubiri huduma kutoka kwenye miradi inayotekelezwa." Amesisitiza Mhe. Mtanda.

Vilevile, amewapongeza Halmashauri hiyo kwa kuongeza wigo wa ukusanyaji wa mapato ya ndani kila mwaka huku akitolea mfano ongezeko la kutoka shilingi Bilioni 17 (2022/23) hadi Bilioni 24 (2023/24) ambayo ni asilimia 88 ya malengo pamoja na uhodari wa kujibu hoja za mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za Serikali.

Naye Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe. Amina Makilagi  pamoja na mambo mengine amebainisha changamoto kadhaa zinazowakabili wananchi kama uhaba wa maji hususani kwa maeneo ya Buhongwa, Lwanhima, Igoma na Butimba na akamuomba kiongozi huyo wa mkoa kushughulikia.

Upungufu wa vyumba vya madarasa 1632, matundu ya vyoo 3807 na madawati 17771 kwa elimu ya awali na msingi ni miongoni mwa changamoto alizozitaja na akabainisha mikakati mbalimbali ya kukabiliana nazo ambazo wanaendelea kushughulikia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.