• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AIPONGEZA BONDE LA ZIWA VICTORIA KWA KUELIMISHA UMMA

Posted on: May 13th, 2025

RC MTANDA AIPONGEZA BONDE LA ZIWA VICTORIA KWA KUELIMISHA UMMA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameipongeza na kutoa maagizo kwa  Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria kuhakikisha Jarida waliloliandaa kuhusu kukabiliana na uvamizi wa Gugumaji jipya katika ziwa victoria (Salvinia Molesta) linawekwa katika mifumo mbalimbali ili jamii iweze kuona, kusoma na kusikiliza vizuri.

Mkuu wa Mkoa ametoa rai hiyo mchana wa leo Mei 13, 2025 alipokuwa akizundua Jarida la Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria linalohusu kukabiliana na uvamizi wa Gugumaji katika Ziwa Victoria ambapo amesisitiza umuhimu wa kuliweka jarida hilo katika mifumo mbalimbali ikiwemo mfumo wa nakala mtandao.

Kadhalika Mkuu wa Mkoa ametoa pongezi kwa Bodi ya Bonde hilo kwa kuja na mpango wa jarida hilo kwa kuwa athari zinazotokana na Gugumaji hilo ni kubwa na inahatarisha uchumi wa Mkoa wa Mwanza na Mikoa ya Kanda ya Ziwa.

“53% ya Mkoa wa Mwanza umezungukwa na ziwa Victoria hivyo hapa Mwanza unapozungumzia maji unazungumzia uchumi, sekta ya usafirishaji, uhifadhi wa mazingira na wavuvi pia”.


kwa hiyo madhara ni makubwa sana na elimu hii mliyoitoa kupitia jarida hili ni muhimu sana kwa jamii na ninawapongeza sana kwa kazi kubwa iliyofanyika lakini bado ni endelevu na ni wajibu wetu kihakikisha kuwa ziwa victoria linaendelea kuwa safi. Ameongeza Mkuu wa Mkoa.

Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria Dkt. Renatus James Shinu amesema Jarida hilo ni maalumu na limelenga kuhakikisha taarifa muhimu ya shughuli, mbinu, na jitihada ambazo zimefanywa na Serikali katika kupambana na Gugumaji hilo ikiwemo na mipango ya baadae inawafikia Wananchi na Wadau wa sekta ya maji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BONDE LA ZIWA VICTORIA KWA KUELIMISHA UMMA

    May 13, 2025
  • RC MTANDA ASISITIZA UIMARISHWAJI WA UMOJA NA MSHIKAMANO

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.