• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ALIVALIA NJUGA TATIZO LA USAFIRI ENEO LA KIVUKO CHA KIGONGO-BUSISI

Posted on: February 2nd, 2025

RC MTANDA ALIVALIA NJUGA TATIZO LA USAFIRI ENEO LA KIVUKO CHA KIGONGO-BUSISI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amelazimika kuamuru mabasi na magari madogo kupita kwenye daraja la muda la mkandarasi eneo la Kigongo Busisi kutokana na kivuko cha MV Sengerema kuharibika injini na kusababisha hali ya uvukaji kuwa mgumu.

Akizungumza na wananchi eneo la kivuko leo Februari 2, 2025 wananchi waliokaa muda mrefu kusubiri kuvuka kuelekea Sengerema na mikoa ya Geita, Kigoma Kagera, Mtanda amesema tatizo hilo limesababishwa na hali mbaya ya magugu maji yaliyotapakaa ziwani humo na kusababisha uharibifu wa injini ya Mv Sengerema.

Amesema tayari amechukua hatua mbili,mosi amefanya mawasiliano na Wizara husika na masuala ya mazingira ili kuwaleta wataalam na wadau wengine wanaopambana na mazingira  kuja kufanya utafiti wa kuyaondoa magugu maji hayo na pili amezungumza na Waziri wa Ujenzi ili alete injini mojawapo inayotarajiwa kufungwa kwenye vivuko vipya vitano vinavyojengwa hapa Mwanza.

"Poleni kwa usumbufu ndugu zangu wananchi tuwe na subira kidogo hali itatengemaa,tayari hatua za msingi nimefanya," amesisitiza mkuu huyo wa mkoa wakati anazungumza na wananchi hao.

Mtanda ambaye amelazimika kusimamia pande zote mbili Kigongo na Busisi upitaji wa magari hayo kwenye daraja la muda la mkandarasi,wasafiri hao walionesha furaha na kumshukuru mkuu huyo wa mkoa kwa kuwakwamua baada ya kusota kwa saa nyingi kusubiri kuvuka.

"Nimekaa hapa kuanzia saa 8 mchana na sikuwa na matumaini ya kuvuka mapema na safari yangu ni Geita,tunamshukuru sana mkuu wa mkoa kwa kutupatia ofumbuzi," Richard Mahizo,msafiri

Kivuko cha Mv Sengerema kimesimama kutoa huduma hii ni wiki ya pili kutokana na injini yake kuharibika na kusalia vivuko viwili vinavyotoa huduma hata hivyo vimee lol elewa kutokana na idadi kubwa ya wasafiri na magari yanayopita eneo hilo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.