Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ARIDHISHWA NA UJENZI WA MIRADI YA KIMKAKATI MWANZA, AMSHUKURU RAIS SAMIA

Posted on: May 17th, 2024

RC MTANDA ARIDHISHWA NA UJENZI WA  MIRADI YA KIMKAKATI MWANZA, AMSHUKURU RAIS SAMIA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo ameendelea na zoezi la ukaguzi wa miradi ya kimkakati akiwa wilayani Nyamagana ameanzia kuona ujenzi wa Soko kuu lililogharimu zaidi ya shs bilioni 23 na kumshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha nyingi ya miradi mbalimbali Mkoani humo, huku akimuhimiza mkandarasi Mohamed Builders kulikamilisha mapema.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema hatua iliyofikia soko hilo ya 94% kabla ya kukamilika ni nzuri na tayari pesa iliyobaki shs bilioni tatu imeshatolewa na Serikali ili Mkandarasi akamilishe na wafanyabiashara waanze kufanya kazi.

"Tuendelee kumshukuru na kumuombea Rais wetu Samia Suluhu Hassan wakati anaingia  madarakani soko hili lilikuwa hatua ya ujenzi asilimia 40  na Mkandarasi akiwa amelipwa 30%,lakini Rais akaongeza asilimia 60 ya malipo yake na sasa tunaona soko limebakiza asilimia 6 kabla ya kuanza kutoa huduma kwa wananchi licha ya kupitia changamoto mbalimbali,asante sana Mhe.Rais,"Mkuu wa Mkoa.

Kaimu Mkuu wa Idara ya Mipango na Uratibu kutoka Halmashauri ya Jiji,Mussa Joram amebainisha soko hilo likikamilika wanatarajia kukusanya mapato ya shs bilioni 3.5 kwa mwaka.

Mkuu wa Mkoa akiwa kwenye mradi wa Hoteli ya nyota 5 inayojengwa na Mfuko wa hifadhi ya Jamii NSSF wenye gharama ya sh bilioni 123 eneo la Capri Point,Mtanda amezihimiza Taasisi zote zinazohusika ikiwemo Tanesco na Mwauwasa kutoa ushirikano ili mradi huo uliofika asilimia 60 ya ujenzi ukamilike kama ulivyokusudiwa Disemba mwaka huu.

Mtanda amesema miradi kama hiyo inahitajika Mkoani humo kutokana na ujenzi wa uwanja wa ndege unaoendelea kufanyika ili uwe wa Kimataifa utaleta wageni wengi hasa watalii.

"Mhe Mkuu wa Mkoa Hoteli hii sasa hivi ipo asilimia 60 ya ujenzi,huduma kamili tunarajia kuanza kutoa Machi mwakani ikiwa na vyumba 195 vya kulala kikiwemo chenye hadhi ya Rais",Emmanuel Kahensa,Meneja NSSF Mwanza.

Mkuu huyo wa Mkoa alipofika kwenye mradi wa Meli ya Mv Mwanza inayojengwa eneo la Mwanza South amewapongeza Kampuni ya huduma za Meli MSCL  kwa kuwa na chombo hicho cha kisasa na kinachoongoza kwa ukubwa ukanda huu wa Afrika eneo la maziwa.

"Huu ni mradi mkubwa sana ambao utachochea uchumi wa Mkoa wetu na Taifa kwa ujumla,Mwanza ni Mkoa uliopo kimkakati eneo la nchi za maziwa makuu,Meli hii ikianza kutoa huduma kupitia nchi za Uganda na Kenya tutazidi kuimarika kiuchumi",Mkuu wa Mkoa

Amesema Meli hiyo itabeba abiria 1200 na tani ya mizigo 400 yakiwemo magari madogo 20 na Malori 3,ni huduma kubwa na ya kisasa ambayo Serikali imegharamia kwa lengo la kuwaletea maendeleo wananchi.

"Meli hii imeigharimu Serikali shs bilioni 123 na Mkandarasi GAS ENTEC ameshalipwa fedha kwa asilimia 91 tunarajia mwishoni mwa mwezi huu tukabidhiwe Meli hii,"Erick Hamis,Mkurugenzi,MSCL

Mhe.Mtanda amekamilisha ziara yake siku ya leo kwa kukagua mradi wa chanzo cha maji eneo Butimba wenye gharama ya zaidi ya shs bilioni 71 na hapo amemshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maji na kuwataka wananchi kuilinda miundombinu ya rasilimali hiyo.

Mtanda amewakumbusha wananchi kujenga tabia ya kulipa ankara za maji kwa wakati ili Serikali izidi kupata fedha na kuwaongezea huduma bora.

"Hongera sana Nelly Msuya kwa hatua hii,mnatekeleza vizuri ilani ya CCM ya kumpatia huduma bora ya maji safi na salama mwananchi.

"Mhe.Mkuu wa Mkoa MWAUWASA tupo mbioni kujenga Matenki makubwa 5 yatakayokuwa na ujazo wa maji lita milioni 31 maeneo ya Fumagila,Buhongwa,Nyamazobe,Kisesa na Usagara lengo ni kuwapatia huduma endelevu ya maji wakazi wa maeneo hayo,"Nelly Msuya,Mkurugenzi MWAUWASA

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.