• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ASHUHUDIA USHUSHAJI WA VIVUKO MAJINI, WANANCHI VISIWANI MKAO WA KULA

Posted on: September 16th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameshuhudia tukio la ushushaji kwenye maji Kivuko cha MV Bukondo kilichogharimu Bilioni 4.7 katika karakana ya Songoro Marine wilayani Ilemela ambayo inatarajiwa kwenda kusafirisha wananchi na mizigo kati ya Kisiwa cha Bukondo na Bwiro wilayani Ukerewe.

Akizungumza baada ya kushuhudia ushushaji huo leo tarehe 16 Septemba, 2025 ambao ni sehemu ya kazi itakayofanyikwa kwa vivuko vinne (4) Mkuu wa Mkoa amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo kujenga vivuko vitakavyosaidia usafiri na usafirishaji.

Amesema, Mwanza yenye eneo la maji kwa asilimia 53 inategemea sana usafiri wa majini hususani kwa wananchi wa visiwani hivyo serikali kuwajengea vivuko vya kisasa itasaidia kuwaondolea adha ya usafiri na hatari ya ajari za majini walizokua wakizipata kutokana na kutumia mitumbwi.

Aidha ametoa wito kwa wananchi kuvipokea na kuvitunza na kwa wataalamau watakaoviendesha amewataka kwenda kufanya kazi kizalendo ili kulinda fedha nyingi ambazo serikali imewekeza kwa ajili ya maendeleo ya wananchi wake.

Mkurugenzi wa vivuko TEMESA Makao Makuu Mhandisi Lukombe King’ombe amesema Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba tani 100, abiria 200 na magari madogo 10 na kwamba ujenzi umefikia  asilimia 98 na mkandarasi amelipwa asilimia 80 ya mradi ambayo ni zaidi ya Bilioni 4.

Ushushaji wa kivuko hicho leo tarehe 16 Septemba, 2025 ni sehemu ya Vivuko 4 kikiwemo cha MV Ukerewe kitakachofanya kazi kati ya Kisiwa cha Rugezi na Kisorya wilayani Ukerewe ambacho kitashusha kesho Septemba 17, 2025 (Zaidi ya Bilioni 6) na vingine vitafuatia na hadi mwezi Novemba vitaanza kutoa huduma.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA ASHUHUDIA USHUSHAJI WA VIVUKO MAJINI, WANANCHI VISIWANI MKAO WA KULA

    September 16, 2025
  • RC MTANDA AWAALIKA WALIOKOSA ELIMU RASMI KUJIUNGA NA MPANGO WA ELIMU WATU WAZIMA

    September 15, 2025
  • RC MTANDA AWATAKIA HERI BENCHI LA UFUNDI PAMBA JIJI FC MSIMU MPYA

    September 12, 2025
  • MAAFISA UFUATILIAJI NA TATHMINI WAASWA KUSIMAMIA MISINGI YA KAZI

    September 12, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.