• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATAKA VITEKENDEA KAZI RUWASA VITUMIKE KUBORESHA HUDUMA ZA MAJI

Posted on: November 6th, 2024

RC MTANDA ATAKA VITEKENDEA KAZI  RUWASA VITUMIKE KUBORESHA HUDUMA ZA MAJI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said

Mtanda amemtaka Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Mkoa wa Mwanza kutumia vitendea kazi vipya na vya kisasa vilivyotolewa kuboresha huduma za maji.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo  Novemba 06, 2024 wakati akikabidhi magari 4 na pikipiki 4 vyenye thamani ya zaidi ya milioni 800 kwenye Ofisi za wakala huo Mkoa ambapo vitatumika kwenye ofisi za mameneja wa Wilaya za Kwimba,  Sengerema na Misungwi.

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha

wananchi wa vijijini wanapata huduma za maji safi kama wapatavyo kwenye maeneo ya miji na ndio maana wanaijengea uwezo RUWASA ili iweze kutekeleza miradi na kuwapatia wananchi huduma hiyo ni lazima watendaji wajitume.

Aidha, amebainisha kuwa tangu Rais Samia aingie madarakani kumekua na ongezeko la hali ya usambazaji maji vijijini kwa asilimia 4 na ni shabaha ya Serikali kuona ifikapo mwaka 2025 wanafikisha asilimia 85 kwa wananchi wa vijijini kama ilani ya CCM ya 2020-25 ilivyosema.

Halikadhalika, amewapongeza RUWASA mkoa huo kwa kufikisha asilimia 72 kwenye usambazaji maji kwa wananchi ambao ni 65% ya wakazi wote na amewasihi kutekeleza vema miradi yote zaidi ya 50 inayoendelea inayogharimu zaidi ya bilioni 146.

Meneja wa RUWASA Mkoa huo Godfrey Sanga ameishukuru Serikali kwa vitendea kazi hivyo na ameahidi kuvitumia kama ilivyokusudiwa na kwa hakika vitakwenda kuongeza huduma kwani vitasaidia kuifikia miradi katika usimamizi.

Aidha, amebainisha kuwa hapo awali walikua wanatumia fedha zaidi ya milioni 300 kukarabati magari chakavu 6 waliyokuwa nayo katika wilaya zote na kwamba kwa sasa ofisi imepata ahueni kwa kupata magari nadhifu na ya kisasa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.