• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AUTAKA UONGOZI WA ATCL KULETA NDEGE ZAIDI MWANZA KUBORESHA USAFIRI

Posted on: July 3rd, 2024

RC MTANDA AUTAKA UONGOZI WA ATCL KULETA NDEGE ZAIDI MWANZA KUBORESHA USAFIRI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda ameutaka uongozi wa Shirika la ndege nchini ATCL kuongeza idadi ya ndege  mkoani humo kutokana na idadi ya abiria kuzidi kuongezeka hali inayosababisha kuwepo na ugumu wa kupata usafiri huo kirahisi.

Mkuu huyo wa Mkoa ametoa rai hiyo leo Julai 03, 2024 wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa chumba maalum cha abiria wa daraja la juu la biashara iliyofanyika eneo la uwanja wa ndege, Mtanda amebainisha kutokana na Jiji la Mwanza kuwa eneo la kimkakati ongezeko la usafiri wa anga limezidi kuongezeka.

"Mkurugenzi Mhandisi Matindi nalisema hili mbele yako, sasa hivi ukitaka kuondoka leo hii kutoka Mwanza kwenda Dar siyo rahisi kupata usafiri ni lazima ufanye utaratibu siku mbili kabla, sasa hii katika soko la ushindani itawaletea shida," amesema Mtanda.

Mkuu huyo wa Mkoa amezitaka Shirika hilo kuzidi kujiimarisha na kuepuka usitishaji wa safari kiholela ili kuzidi kujiaminisha kwa huduma bora kwa wateja wake, kwani mashirika makubwa ya kimataifa ndege yatakapoanza safari zake kuanzia uwanjani hapo waweze kuumudu ushindani.

"Nampongeza Rais Samia kwa kuendeleza mazuri kwenye Shirika hilo yaliyofanywa na watangulizi wake, ametoa shs bilioni 13 kujenga jengo la kisasa la abiria, hivi sasa mkandarasi Taifa yupo eneo la ujenzi kulikamilisha jengo hilo litakalo chukua abiria wa kigeni 600 kwa mkupuo na wazawa 800," Mhe. Mtanda.

Aidha Mtanda amelishauri ATCL kuona umuhimu wa kuweka safari ya moja kwa moja kutoka Mwanza hadi Makao makuu ya nchi Dodoma, kuliko ilivyo sasa abiria kulazimika kushukia Dar na kwenda Dodoma.

"Haiwezekani kushindwa kuwepo na muunganiko wa safari ya moja kwa moja kwenda makao makuu ya nchi ni lazima muone hadhi ya Dodoma na wapo abiria wengi wanaohitaji usafiri huo," amehimiza Mtanda wakati wa hafla hiyo fupi.

Mkurugenzi Mkuu wa ATCL Mhandisi Ladislaus Matindi amesema wanatambua mchango mkubwa wa kibiashara wa Mkoa wa Mwanza na wapo katika mkakati wa kuboresha usafiri kutokea mkoani humo

"Hivi sasa tuna ndege 14 na tupo mbioni kupata ndege nyingine moja, tuna imani changamoto zilizopo zitamalizika na huduma zetu zitazidi kuimarika", amesema Mhandisi Matindi.

ATCL iliyoanzishwa mwaka 1977 baada ya kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, wameingia mkataba wa huduma hiyo ya chumba cha daraja la juu la abiria wa biashara na VIA Aviation kwa miaka 2 na wapo mbioni kuanzisha huduma hiyo uwanja wa ndege wa Dodoma.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.