• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWAKARIMU MADIWANI KUTOKA ARUSHA JIJI

Posted on: September 17th, 2024

RC MTANDA AWAKARIMU MADIWANI KUTOKA ARUSHA JIJI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo septemba 17, 2024 amewatembelea Wahe. Madiwani, Wataalamu na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha waliowasili Mkoani Mwanza kwa ziara ya kikazi na kujifunza mambo mbalimbali.

Mhe. Mtanda amekutana na Wahe. Madiwani hao katika Ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza na kuwakaribisha Mwanza kisha kuwataka kutembelea maeneo mbalimbali ya kiutalii ili watakaporudi Mkoani Arusha wakayaelezee yale yote mazuri waliyokutana nayo Mkoani Mwanza.

Mkuu huyo wa Mkoa amesema Mwanza ni Mkoa mkubwa namba mbili kwa idadi ya watu pamoja na muingiliano wa shughuli nyingi za kiuchumi hivyo kuchagua Mkoa wa Mwanza hawajakose kwani ni eneo sahihi la kujifunzia, na kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Waheshimiwa hao ambao pia wengi wao anafahamiana nao kwa kuwa aliwahi kufanya nao kazi wakati alipokuwa Mkuu wa Wilaya ya Arusha mwaka 2021 - 2023.

Sambamba na hayo amewataka Wahe. hao kama watapata nafasi wasisite kutembelea miradi ya kimkakati inayotekelezwa katika Mkoa wa Mwanza ambayo serikali imetoa fedha nyingi kuhakikisha miradi hiyo inatekelezeka ili kurahisisha huduma kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza, Mikoa jirani pamoja na Nchi jirani.

Naye Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Arusha Mhe. Maximilin Iranqe amemshukuru Mhe. Mtanda kwa ukarimu wake na kutenga muda kuwatembelea Waheshimiwa hao licha ya kuwa na ratiba ngumu, Aidha amemuhakikishia kuwa wataenenda kama alivyowashauri na kumalizia kwa kumtaka kuendelea kushirikiana nao kwa kipindi chote watakapowepo Jijini humo.

Wahe. Madiwani pamoja na Wataalamu hao wamefika Mwanza kwa lengo la kujifunza; Usimamizi na uendeshaji wa stendi ya Nyamhongolo, Uendeshaji wa vikao kwa mfumo wa e-board, Uendeshaji wa jengo la kibiashara la Rock City Mall, Usimamizi na ukusanyaji wa leseni za biashara, kodi ya pango na ushuru wa nyumba za kulala wageni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.